Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, July 26, 2009

YANGA - HATUENDI MWANZA NG`O!!! KAMBI YAWEKWA YANGA HOUSE

Hili ni jengo la Yanga (YANGA HOUSE)likkiwa katika ukarabati mkubwa wa kuhakikisha linakuwa la kibiashara na kupunguza gharama za klabu kuweka kambi.
Katika harakati za kujiandaa na ligi kuu ya msimu ujao Uongozi wa klabu ya Yanga umesema hauna sababu yoyote ya kwenda sehemu nyingine kuweka kambi kwani tayari jengo lao limeshakamilika kwa asilimia tisini na tano.
Iman Mahugira Madega ni mwenyekiti wa timu hiyo yenye maskani yake jangwani Jijini Dar es salaam amesema taarifa za kambi ya klabu hiyo kwenda Mwanza si za kweli na sasa wataweka kambi katika jengo la klabu hiyo na wanafanya kila jitihada pamoja na uwanja ukamilke haraka ili uweze kutumika katika michezo yao ya ligi kuu.
Madega ameongeza kuwa mpaka sasa zaidi ya shilingi bilioni moja nukta mbili zimekwishatumika ambapo kuna vyumba vya kulala ishirini na tisa ambapo kila chumba watalala wachezaji wawili wawili pamoja na sehemu ya kuogelea swimming pool na sehemu za kupumzikia.
Akizungumzia kuhusu katibu ,mhasibu na msemaji wa kuajiriwa amesema suala hilo lipo kwenye mchakato wa kutafuta watendaji hao kwani wanafahamu kuwa hawataweza kushiriki ligi kuu bila ya kutekeleza agizo hilo la Tff.

No comments :

Post a Comment