Kufuatia sare hiyo Yanga sasa wamejikusanyia pointi 5 tangu kuanza kwa ligi ikiwa tayari wamekwishacheza michezo minne, huku wakiwa na rekodi ya kushinda mchezo mmoja dhidi ya Manyema, sare mbili katika mchezo dhidi ya African Lyon na JKT Ruvu na kupoteza mchezo mmoja dhidi ya Maji Maji.
JKT Ruvu hadi sasa wamejikusanyia pointi 7 wakiwa na rekodi ya kushinda michezo miwili dhidi ya Tanzania Prison na Maji Maji, na kufungwa mchezo mmoja na Mtibwa na sare moja dhidi ya Yanga.
No comments :
Post a Comment