Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Wednesday, December 14, 2011

MOTO KUWAKA DDC KEKO DESEMBA 24



BONDIA wa ngumi za kulipwa nchini, Venance Mponji,a anatarajia kuzichapa na mpinzani wake Chaurembo Palasa, katika pambano la kuwania ubingwa wa TPBC wa Afrika litakalopigwa Desemba 24 mwaka huu katika Ukumbi wa DDC Keko, Dar es Salaam.

Akizungumza Dar es Salaam , Promota wa pambano hilo, Kaike Siraji, alisema kuwa wameandaa pambano hilo ili kuweza kumaliza ubishi uliopo kati ya mabondia hao.

Alisema kuwa pambano hilo linatarajiwa kuwa la aina yake kwani mabondia hao wameshakutana mara mbili ambapo kila bondia ameshinda mara moja.

Kaike alisema kuwa pambano hilo linatarajiwa kuwa la uzito wa Light Walter ambalo litakuwa la raundi 12.

Alisema kuwa pia katika pambano hilo kutakuwa na mapambano mbalimbali ya utangulizi ambayo yatashirikisha mabondia wa uzito tofauti tofauti.

“Tumeandaa pambano la aina yake ambalo litaweza kuondoa ubishi na bingwa wa pambano hilo, nitamtafutia pambano la kimataifa ambapo atazichapa na bondia kutoka New Zealand ambapo pambano hilo litafanyika hapa nchini mapema mwakani” alisema.

Aliwataja mabondia wengine watakaozichapa katika pambano hilo kuwa ni pamoja na Baina Mazora ambaye atazipiga na Juma Fundi katika pambano la uzito wa Bantam la raundi nane, pambano lingine litawakutanisha Seba Temba na Said Zungu litakalokuwa la raundi sita katika uzito wa Light.

Wengine ni Fred Sayuni ambaye atazichapa na mpinzani wake Simba Tunduru katika pambano la uzito wa Bantam la raundi sita na Mainya Ramadhan atapigana na Mikidadi Tyson katika pambano la raundi sita katika uzito wa Light Weight

Mbali na kuwepo mapambano ya ngumi kutakuwa na uuzwaji wa DVD zenye mapambano ya mabingwa wa Dunia akiwemo Manny Paquaio, Floyd Maywherth, Roy Jones na wengine kiba DVD hizo zilizoandaliwa kwa ubora wa hali ya juu zitakuwa zikiuzwa kwenye mpambano huo na Kocha Rajabu Mhamila 'Super D', alisema kuwa kutakuwa na DVD ili kuweza kuwauzia mashabiki kwa ajili ya kujifunza Kanuni na Sheria za mchezo huo.

"Ninatarajia kuwapelekea DVD mashabiki wa ngumi watakaokuwepo katika pambano la Cheka na Maugo ili kuweza kujifunza mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na sheria za mchezo wa ngumi", alisema Super D

No comments :

Post a Comment