Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, April 29, 2012

SIMBA KUIVAA AL AHLY SHANDY YA SUDAN LEO UWANJA WA TAIFA DAR ES SALAAM.



Wawakilishi pekee waliobaki toka Klabu za Tanzania katika michuano ya Barani Afrika, Simba, leo wanatinga Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kucheza Mechi ya kwanza ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya michuano ya CAF ya Kombe la Shirikisho kwa kucheza na Al Ahly Shandy ya Sudan.

Katika Raundi zilizopita, Simba walibwaga Kiyovu ya Rwanda kwa jumla mabao 3-2 katika Mechi mbili kisha kuwatoa ES Setif ya Algeria kwa bao la ugenini baada ya kufungana bao 3-3 katika Mechi mbili, Simba wakishinda Dar es Salaam bao 2-0 na kuchapwa 3-1 huko Mjini Setif, Algeria.

Nao Al Ahly Shandy waliwatoa Ferroviario de Maputo ya Msumbiji Raundi iliyopita na ingawa Klabu hii ya Sudan ni mara ya kwanza kucheza michuano ya Klabu Afrika lakini kwa mchezo ilioonyesha walipocheza na Ferroviario de Maputo na kushinda 1-0 ugenini Maputo na 2-0 kwenye Mechi ya marudiano, Timu hii si ya kubeza.

Timu hizi zitarudiana hapo Jumamosi Mei 12 huko Mjini Shandy, Mji ambao uko Kilomita 150 Kaskazini Mashariki ya Mji Mkuu wa Sudan, Khartoum.

Na katika mechi hiyo kiingilio cha chini ni sh 5,000/=
You might also like:

No comments :

Post a Comment