Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, April 24, 2012

TEWUTA IMEWATAKA TCRA KUPUNGUZA TOZO INAYOLIPWA NA MAKAMPUNI YA SIMU NCHINI.


(NA VERONICA KAZIMOTO – MAELEZO)
DAR ES SALAAM

 Chama cha Wafanyakazi wa Sekta ya Huduma za Mtandao wa Mawasiliano Tanzania (TEWUTA) kimeitaka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TICRA), kupunguza tozo inayolipwa na makampuni ya simu nchini.
 
Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dare s Salaam leo, Katibu Mkuu wa chama hicho Junus Ndaro amesema TCRA imeshindwa kusimamia na kuhakikisha gharama za huduma za mawasiliano ya simu zinapungua na kuwa na uwiano sawa kwa tozo za makampuni yote Tanzania.
 
“Mamlaka imeshindwa kuwaeleza watanzania kwa uwazi na huku ikitambua kuwa moja ya jukumu lake ni kupanga bei elekezi kwa makampuni ya simu, kitendo ambacho hakijafanyika toka mamlaka hiyo iundwe na kutangazwa kwenye vyombo vya habari”, amesema Ndaro.
 
Ameongeza kuwa pamoja na mambo mengine chombo hiki kiliundwa kwa madhumuni ya kumsaidia mteja kupata bei nafuu kila anapotumia mtandao wowote wa simu.
 
“Ni ukweli kuwa watanzania wamechoka kutembea na simu zaidi ya moja za mitandao tofauti kwa sababu ya kutafuta punguzo kwa mtandao husika, hivyo ni wajibu wa TCRA kusimamia mitandao yote ya simu nchini kuwa na bei zenye uwiano wa karibu” amesisitiza Ndaro.  
Ndaro amesema kuwa serikali imeleta Mtandao wa Mkongo (FIBRE) ambao gharama zake za uendeshaji ni mdogo sana na unafanya kazi vizuri kwa haraka zaidi hivyo kuna uwezekano mkubwa kwa TCRA kupunguza gharama wanazotoza kutoka kwenye makampuni ya simu.

No comments :

Post a Comment