Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, April 14, 2012

TBL WADHAMINI WAPYA TAIFA STARS



BIA ya Kilimanjaro Premeum Lager rasmi ndio mdhamini mpya wa timu ya taifa ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, bongostaz imeipata hiyo.
Bia hiyo inayozalishwa na kampuni ya Bia Tanzania (TBL), wiki hii itafanya hafa maalum ya kuutangaza rasmi udhamini huo.
Chanzo cha habari kutoka TBL, kimesema hafla hiyo itafanyikia katika hoteli ya Serena, iliyokuwa Royal Palm Movenpick, Dar es Salaam wiki hii.
Tangu mwaka 2006, Taifa Stars imekuwa ikidhaminiwa na Serengeti Breweries Limited ambao wameshindwa kuingia mkataba mpya na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kwa sababu ya kupandishiwa dau.
Baada ya mkataba wao (SBL) kufikia tamati Desemba, mwaka jana, TFF ikaipandishia dau la udhamini kutoka Sh. Bilioni 1.2 hadi Bilioni 3.6, ambayo ni zaidi ya asilimia 300.
TBL imekubali kuidhamini Stars kwa dau la Sh. Bilioni 3.6 kwa mwaka.
Kilimanjaro pia ni wadhamini wa watani wa jadi katika soka ya Tanzania, Simba na Yanga na mashindano ya Kombe la Taifa, Kili Taifa Cup.

No comments :

Post a Comment