Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, October 10, 2014

BENKI YA POSTA YAZING'ARISHA TASWA FC NA TASWA QUUENS




Meneja mahusiano mwandamizi wa Benki ya Posta Tanzania (TPB) Noves Moses (kushoto) akimkabidhi jezi nahodha wa timu ya netiboli ya waandishi wa habari za michezo nchini (Taswa Queens) Imani Makongoro (Kulia) katika halfa fupi iliyofanyika makao makuu ya benki hiyo jana. Katikati ni Mwenyekiti wa Taswa SC, Majuto Omary . Picha/Mpigapicha wetu
*****************************************
Na Mwandishi Wetu, Dar
Benki ya Posta Tanzania (TPB) imeendelea kuisadia  timu ya   Waandishi wa habari za  michezo nchini (Taswa SC) baada ya kuikabidhi vifaa vya michezo kwa ajili ya kutumika katika mashindani na michezo mbali mbali ya kirafiki.
Benki hiyo imekabidhi seti za jezi kwa timu hizo zikiwa na jumla ya thamani ya Sh1,180,000 kwa timu ya mpira wa miguu maarufu kwa jina la Taswa FC na timu ya netiboli ambayo pia inajulikana kwa jina la Taswa Queens.
Akizungumza katika makabidhiano hayo, Meneja mahusiano mwandamizi wa Benki ya Posta Tanzania (TPB) Noves Moses alisema kuwa msaada huo ni sehemu ya shughuli za benki kijamii na kutambua mchango mkubwa wa waandidshi wa habari hapa nchini.
“Waandishi wa habari wameonyesha mfano mkubwa kwa kucheza soka na netiboli, pia niliona mnafanya mazoezi ya ngumi chini ya bondia Thomas Mashali, huu ni mfano wa kuigwa na ndiyo maana tumevutiwa na utendaji na maendeleo yenu,” alisema Noves.
Mwenyekiti wa Taswa SC, Majuto Omary aliishukuru TPB kwa kuendelea kuwakumbuka na kuahidi kutumia jezi hizo kwa kushinda mechi na wala si kutoka sare au kufungwa.
“Tunajivunia uwepo wa Benki ya Posta kwa kuthibitisha kuwa ni benki halisi ya Watanzania, nachukua fursa hii kuwaomba Watanzania kufungua akaunti zao katika benki hii na vile vile kuomba wadau wengine kufuata mfano wao kwa kuisaidia Taswa SC ili iweze kufanikisha ziara zake,” alisema Majuto.

No comments :

Post a Comment