Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, October 14, 2014

Dk Ndumbaro yamkuta, afungiwa miaka 7 katika soka



BAADA ya tetezi zilizokuwa zikizagaa kwamba huenda Mwanasheria wa klabu za Ligi Kuu Tanzania Bara, Dk Damas Ndumbaro yupo kitanzini na huenda akaadhibiwa kwa kauli alizotoa hivi karibuni kuhusiana na makato ya 5% zilizotakiwa na Shirikisho la Soka Tanzania, TFF, hatimaye imethibitika kuwa kweli.
Kamati ya Nidhamu ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imemfungia Dk Ndumbaro kujihusisha na mambo ya soka kwa muda wa miaka saba na faini ya kiasi cha fedha.
Ndumbaro ambaye aliingia katika mzozo mkubwa na Rais wa TFF, Jamal Malinzi wiki iliyopita baada ya TFF kuagiza kila klabu kukatwa asilimia tano za mapato yatokanayo na udhamini wa klabu hizo wanaoupata kutoka kwa Vodacom, wadhamini wakuu wa ligi kuu ya Tanzania Bara, na Azam TV.
Ndumbaro alikimbilia katika vyombo vya habari na kusema wazi kuwa, klabu zimemuagiza kuwaambia TFF kuwa havipo tayari na havitakubali jambo hilo litokee, huku akijiamini na kuchambua baadhi ya vipengele na mambo ya sheria, Ndumbaro alivuka mipaka pale aliposema kuwa wanatafuta wastani wa wajumbe wa mkutano mkuu wa TFF na kupiga kura ya kutokuwa na imani na rais wa shirikisho, Malinzi.
Kikao cha juzi cha kamati ya nidhamu kimefikia uamuzi wa kumfungia, Ndumbaro na kumlilipisha faini kwa sababu, Ndumbaro ambaye alizungumza kama wakili wa klabu za ligi kuu kupitia,.
TFF imedai Ndumbaro amekanwa na klabu ingawa taarifa zinaeleza si kweli kwa kuwa viongozi wa klabu 12 walisaini kumpitisha kuwa wakili wao

No comments :

Post a Comment