Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, October 11, 2014

Rais Kikwete afungua jengo la PPF Mwanza


Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akikata utepe kufungua rasmi jengo la kitega uchumi la mfuko wa pensheni la PPF mjini Mwanza jana jioni.Wengine katika picha kutoka kushoto,ni Waziri wa Ujenzi Dkt.John Pombe Magufuli, Mkurugenzi Mkuu wa PPF Bwana Wiliam Erio, Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Adam Malima, Mwenyekiti wa Bodi ya PPF Bwana Ramadhani Kija, na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evaristi Ndikilo.
Jengo la Kitega uchumi la mfuko wa pensheni wa PPF lililozinduliwa rasmi na Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete mjini Mwanza jana jioni.
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete na Mkurugenzi Mkuu wa PPF Bwana William Erio wakiangalia madhari nzuri ya jiji la Mwanza wakiwa katika jengo jipya la kitega uchumi la mfuko wa pensheni wa PPF muda mfupi baada ya kulizindua mjini Mwanza jana jioni.
Naibu Waziri wa Fedha Adam Malima, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya PPF Bwana Ramadhani Kija(watatu kushoto), na Mkurugenzi Mkuu wa PPF Bwana William Erio(kulia) wakimkaribisha Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete kuzindua jengo la kitega uchumi la PPF mjini Mwanza jana jioni.
Mkurugenzi Mkuu wa PPF Bwana William Erio akitoa maelezo kwa Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete ndani ya mgahawa uliopo katika jengo jipya la kitega uchumi la PPF muda mfupi baada ya kulizindua rasmi mjini Mwanza.Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhandisi Evarist Ndikilo.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa pamoja na viongozi na wafanyakazi wa Shirika la PPF baada ya kuwa amezindua Jengo la Kitega Uchumi la Shirika hilo katikati ya Jiji la Mwanza jana, Ijumaa, Oktoba 10, 2014. Rais Kikwete yuko katika ziara ya siku tatu ya kikazi Mkoani Mwanza.(picha na Freddy Maro)

No comments :

Post a Comment