
Hivi 
karibu Msanii Mahiri na Nguli katika tasnia ya filamu nchini Elizabeth 
Michael almaarufu kama LULU ataibuka na filamu yake Mpya na yenye 
kusisimua iitwayo "MAPENZI YA MUNGU" 
ambapo moja kati ya washiriki katika filamu hiyo ni Bi Flora Mtegoha 
ambae ni Mama Mzazi wa aliyekuwa Msanii Nguli wa Kiume Hapa Bongo 
Marehemu Steven Kanumba.
Filamu ya "Mapenzi ya Mungu"
 ni moja ya filamu ambayo Lulu ameonyesha uwezo wa hali ya na 
kuthibitisha kuwa ni mmoja kati ya wasanii wa kike hapa Tanzania ambae 
ana kipaji cha hali ya juu katika kuuvaa uhusika ambapo ana uwezo wa 
kubadilika badilika kutokana na muongozo anaopewa.
Filamu ya "Mapenzi ya Mungu" itakuwa Sokoni hivi Karibu Kwa Wauzaji wa Filamu kote Nchini.
Filamu hii itasambazwa na Kampuni mahiri ya Proin Promotions Ltd.
No comments :
Post a Comment