Timu ya Bussiness Times Limited maarufu The Bize ikiwa ni wamiliki wa gazeti la majira, Dar Leo, Spoti Starehe, Bussines Times na Radio Times FM leo wamefanikiwa kutnga hatua ya robo fainali ya michuano ya kombe la NSSF.
The Bize imefanikiwa kutinga robo fainali baada ya kuizaba Radio Kheri kwa magoli 2-0.
Mchezaji Rehure Nyaulawa ambaye ni mkurugenzi wa Radio Times FM ndiyo alikuwa wa kwanza kuwanyanyua mashabiki wa The Bize baada ya kufunga goli kwanza katika dakika ya 60 kipindi cha pili.
Kama haitoshi mchezaji Sande George alifunga goli la pili na la ushindi katika dakika ya 75 ya mchezo.
Ushindi huo mnono wa The Bize ulitokana na namna ambavyo walilisakama lango la radio Kheri na kuhakikisha wizara ya Ulinzi haitoi nafasi ya mchezaji yeyote kukutana wala kusalimiana na golikipa wa The Bize.
baada ya ushindi huo wa The Bize sasa watakutana na timu ya NSSF ambao ni wenyeji wa mashindano hayo katika mchezo wa robo fainali hapo siku ya Jumatatu ya tarehe 15 mwezi Machi, 2010.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment