Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, March 23, 2010

TFF - SIMBA, TAIFA STARS NA TWIGA STARS WAWAKILISHA KIMATAIFA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TIMU YA TAIFA - TWIGA STARS
Twiga Stars imefaulu kusonga mbele katika mashindano ya kuwania kufuzu kwa fainali za saba za Afrika kwa wanawake zitakazofanyika Afrika Kusini baadaye mwaka huu baada ya kuitoa Ethiopia kwa ushindi wa jumla ya magoli 4-2.
Ni dhahiri kuwa ushindi huo umetokana na kujituma kwa wachezaji, mbinu sahihi za mwalimu na wasaidizi wake wa jopo la ufundi pamoja na matunzo ambayo timu hiyo ilipewa wakati wakijiandaa na mchezo huo na jamii kwa jumla.
Twiga Stars bado inakabiliwa na michezo miwili dhidi ya Eritrea ambapo mchezo wa kwanza utafanyika hapa nyumbani tarehe 22 Mei 2010 na mchezo wa marudiano utafanyika majuma mawili baadaye huko Asmara.
TFF inafahamu umuhimu na ina nia thabitri ya kuandaa timukikamilifu pale inapokabiliwa na mashindano.
Timu zote za Taifa zimekuwa zikitayarishwa katika mazingira ya kuridhisha kulingana na hali halisi iliyopo.
Katika hali hhii Twiga Stars, kama ilivyo kwa timu nyingine zisikuwa na udhamini wa kimkataba itaendelea kuandaliwa vizuri kulingana na hali halisi.Tunapenda pia kwa mara nyingine kuomba makampuni ya kibiashara, taasisi mbali mbali, serikali na jamii kwa jumla kuisaidia timu hii ili iweze kuliwakilisha vema taifa.
TFF tayari imeanza mazungumzo na makampuni kadhaa juu ya utekelezwaji wa programu ya mwalimu Charles Boniface Mkwasa.

2. USHIRIKI WA TIMU YA SIMBA KATIKA MASHINDANO YA KIMATAIFA

Timu ya Simba imefanikiwa kupata ushindi mkubwa wa magoli 3-0 ugenini dhidi ya timu ya Lengthens ya Zimbabwe katika kombe la shirikisho.
TFF inapenda kuwapongeza Simba ambao ni wawakilishi pekee wa nchi waliosalia katika michuano ya kimataifa.
Tunafahamu fika kuwa bado kuna mchezo wa marudiano utakaofanyika kati ya tarehe 3 na 4 April 2010, ambao Simba wanahitaji kufanya vema ili kuendelea kulinda heshima ya nchi.
TFF inapenda kuwahakikishia simba kuwa itashirikiana kwa kila hali na simba ili kuhakikisha wanafanya vema kwenye mchezo huo na mingine itakayofuata.

3. TIKETI ZA KOMBE ;A DUNIA 2010.
Kama tulivyotangaza awali FIFA iliitengea Tanzania tiketi 290 Kombe la Dunia litakalofanyika Afrika Kusini Juni hadi Julai 11, 2010.
Ladhalika tilitangaza kuwa watu wote walikuwa wameomba kununua tiketi hizo wazilipe ili kwa fedha ziwasilishwe FIFA na hatimaye tiketi zitumwe nchini.
Tunapenda kuutangaza umma kuwa tumefanikiwa kuuza tiketi zote 290 ambazo FIFA iliitengea Tanzania.
Tiketi zilizouzwa zinathamani ya Dola za Marekani 62,710. Fedha hizo tayari zimetumwa FIFA ili waweze kuleta zilizonunuliwa.
TFF inawashukuru wote waliolipia tiketi zao walizoomba.
Tumewaandikia tena FIFA kuwaeleza na kuwakumbusha kuwa maombi tuliyokuwa nayo yalikuwa mengi kuliko mgawo wa tiketi walizotupatia hivyo watufikirie katika tiketi za nyongeza tulizoomba. Matarajio ni kwamba watatufikiria kjwa kuzingatia idadi ya tiketi zilizonunuliwa kwenye mgawo.

4 TIMU YA TAIFA - TAIFA STARS

Taifa Stars inahceza na timu ya Taifa ya Somalia Jumamosi hii Machi 27, 2010 katika mchezo wa kuwania kufuzu kwa fainali za Afrika kwa wachezaji wa ligi za nyumbani zitakazofanyika Sudan Januari 2011.
Taifa Stars inaendelea na kambi yake chini ya mwalimu Marcio Maximo na mazoezi yanakwenda vizuri tayari kwa kuwakabili wa Simalia.
Mchezo dhidi ya Somalia unachezwa mmoja tu kwa vile Somalia iliiomba Tanzania na CAF kutokana na Shirikisho la Mpira wa miguu la Somalia kutokuwa na uwezo wa kuandaa mchezo wa nyumbai huko Djibout, ifahamike kuwa Somalia kwenyewe hakuna mazingira ya kucheza mashindano ya kimataifa.
Kwa hiyo mchezo huo wa Jumamosi lazima utoe mshindi na kama mshindi hatakuwa amepatikana baada ya dakika tisini (90) itabidi itumike changamoto ya mikwaju ya penati kumpata mshindi.
Mshindi atacheza na Rwanda. Iwapo Taifa Stars itafaulu kusonga mbele itaanza nyumbani dhidi ya Rwanda hapo Mei Mosi badala ya Mei 22. Hii ni kufuatia CECAFA kuiomba CAF Kurejesha nyuma michezo ya kufuzu kwa CHAN kwa ukanda huu ili kutoa fursa ya kuchezwa kwa kombe la Kagame kuanzia Mei 15 - 29.
Kwa sasa yanangonjewa mawasiliano ya CAF.
Mchezo wa Somalia utafanyika uwanja wa Uhuru kuanzia saa tisa 9 Alasiri.

Viingilio

Viingilio vimewekwa katika makundi manne kama ifuatavyo:

VIP (RANGI YA BLUU) - 30,000/=
Jukwaa kuu - Nyekundu & Njano - 15,000/=
Jukwa la kijani - 10,000/=
Mzunguko - 3,000/=

Waamuzi

Waamuzi wanatokea Kenya, Mwamuzi wa kati ni Kirwa Sylvester, msaidizi wa kwanza ni John Ngururi, msaidizi wa pili ni Range Marwa Aden wakati msaidizi wa akiba Israel Mujuni Nkongo wa Tanzania. Kamishna ni Hussein Fadoul wa Djibout.
Timu ya Somalia inatarajiwa kuwasili Alhamisi saa saba mchana kwa ndege ya shirika la ndege la Ethiopia na itakuwa na msafara wa watu 25.
TFF inawaomba watanzania kujitokeza kwa wingi siku ya Jumamosi kuiunga mkono mkono timu ya taifa ili iweze kufanya vema katika harakati za kufuzu kwa mara ya pili mfululizo.
Kwa fainali za Afrika kwa wachezaji wa ligi za nyumbani (CHAN).

Fredrick mwakalebela.
KATIBU MKUU - TFF

No comments :

Post a Comment