Chelsea imeondolewa katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya baada ya vijana wa Jose Mourinho, Internazionale kuibuka na ushindi wa goli 1-0 katika dimba la Stamford Bridge na kufanikiwa kutinga hatua ya robo fainali kwa jumla ya magoli 3-1.
Inter imekuwa ikitolewa katika hatua ya mtoano ambayo hujumuisha klabu 16 katika ligi ya mabingwa barani Ulaya katika kipindi cha misimu mitatu mfululizo, tena ikiotolewa na klabu za Uingereza mara mbili, lakini Samuel Eto'o kunako dakika 79 ilitosha kuwaondosha Chelsea nje ya ligi ya mabingwa.
Didier Drogba alijikuta akitolewa kwa kadi nyekundu dakika tatu kabla ya mpira kumalizika kufuatia kumchezea Thiago Motta.
Makocha wote wawili walifanya mabadiliko, kocha Mourinho alimuingiza Goran Pandev na kufanya safu ya ushambuliaji kuwa na wachezaji wa tatu ikiwa ni pamoja na Eto'o na Diego Milito, wakati Carlo Ancelotti alimuingiza mlinzi Paulo Ferreira pamoja na Yuri Zhirkov.
Golikipa nambari tatu wa Chelsea Ross Turnbull alikaa golini ikiwa ni mchezo wake wa tatu akiwa amaevalia jezi ya Chelsea.
Mdau wa viwanjani anawapa Pole mashabiki wa Chelsea na kuwapongeza mashabiki wa Inter MilanDidier Drogba akimuomba msamaha Mwamuzi baada ya kumlima kadi nyekundu.Makocha kazini, Morinho naye anambwembwe?
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment