
Inter imekuwa ikitolewa katika hatua ya mtoano ambayo hujumuisha klabu 16 katika ligi ya mabingwa barani Ulaya katika kipindi cha misimu mitatu mfululizo, tena ikiotolewa na klabu za Uingereza mara mbili, lakini Samuel Eto'o kunako dakika 79 ilitosha kuwaondosha Chelsea nje ya ligi ya mabingwa.
Didier Drogba alijikuta akitolewa kwa kadi nyekundu dakika tatu kabla ya mpira kumalizika kufuatia kumchezea Thiago Motta.
Makocha wote wawili walifanya mabadiliko, kocha Mourinho alimuingiza Goran Pandev na kufanya safu ya ushambuliaji kuwa na wachezaji wa tatu ikiwa ni pamoja na Eto'o na Diego Milito, wakati Carlo Ancelotti alimuingiza mlinzi Paulo Ferreira pamoja na Yuri Zhirkov.
Golikipa nambari tatu wa Chelsea Ross Turnbull alikaa golini ikiwa ni mchezo wake wa tatu akiwa amaevalia jezi ya Chelsea.
Mdau wa viwanjani anawapa Pole mashabiki wa Chelsea na kuwapongeza mashabiki wa Inter Milan


No comments :
Post a Comment