Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, March 16, 2010

ULINZI STARS YASHIKILIA USUKANI WA LIGI KUU KENYA

Klabu ya Kenya, Ulinzi Stars, ambayo haijapoteza mchezo hata mmoja tangu kuanza kwa msimu wa ligi kuanza, sasa inaongoza ligi kuu ya Kenya (Kenya Premier league) ikiwa na jumla ya pointi 10, ikiwa pointi moja mbele dhidi ya KCB ambayo imefanikiwa kushinda michezo mitatu na kupoteza mchezo mmoja.
Klabu ya Western Stima inashika nafasi ya tatu ikiwa na jumla ya pointi 8, moja zaidi ya timu inayoshika nafasi ya nne klabu ya Sher Karuturi na pointi mbili mbele ya klabu kongwe ya Tusker na kukamilisha klabu tano ambazo zimekuwa na matokeo mazuri tangu kuanza kwa ligi.
Mathare United ilipata ushindi wake wa kwanza msimu huu katika mchezo wa jumapili kwa kuifunga Posta Rangers 2-1 na kujikuta ikilala nafasi ya sita ikilingana pointi na Tusker pamoja na Nairobi City Stars, Sony Sugar na AFC Leopards ambao wanashika nafasi ya 7 hadi 9 katika msimamo.
Mabingwa watetezi, klabu ya Sofapaka, ambao walipata pointi katika mchezo wa jumatatu dhidi ya Mahakama, sasa inashika nafasi ya 10 katika msimamo ikiwa na pointi nne.
Nafasi ya 11-13 inashikiliwa na Mahakama, Gor Mahia na Thika United ambazo zinapointi tatu kila moja, wakati Chemilil Sugar na Posta Rangers zinapointi moja moja na kushika nafasi ya 14 na 15.
Klabu ya Red Berets inashikilia mkia wa ligi kuu ya Kenya wakiwa na pointi moja mkononi.

No comments :

Post a Comment