Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, March 19, 2010

TFF YAONGEA DHIDI YA KUKAMATWA KWA TIKETI BANDIA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
19/03/2010

Jumatatu tarehe 15/03/2010 wakati wa mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom kati ya Yanga na Moro United uliofanyika uwanja wa Uhuru Dar es Salaam, mmoja wa wauza tiketi, Mohamed Baruani alikutwa na kitabu kimoja cha tiketi ambacho hakikuwa miongoni mwa vitabu vilivyokabidhiwa rasmi kwa wauzaji wa tiketi.Wakati akihojiwa muuzaji huyo alisema alikabidhiwa kitabu hicho cha tiketi na mmoja wa maofisa wa TFF wanaohusika na masuala ya tiketi.
Kutokana na hali hiyo maofisa wa Polisi waliendelea kufuatilia ikiwemo kuwahoji wahusika.
Miongoni mwa hao waliohojiwa na kwa maana hiyo wanalisaidia jeshi la polisi, ni afisa wa TFF Daniel Msangi pamoja na baadhi ya watendaji wa kiwanda cha Inter Press of Tanzania Limited, ambao ni wachapishaji wa tiketi za mchezo kati ya Yanga na Moro United.
Kwa mantiki hiyo suala hili lipo mikononi mwa Polisi na linashughulikiwa kwa mujibu wa taratibu za kisheria.
TFF inashukuru na kuwapongeza wale wote waliotoa taarifa ambazo baadaye zilifanikisha kubainika uwepo wa kitabu kilicho nje ya utaratibu na inaahidi kwa dhati kuwa itatoa kila aina ya ushirikiano kwa jeshi la Polisi katika kushughulikia jambo hili.
Kwa kuwa tukio hili bado limo mikononi mwa Polisi na linafanyiwa kazi kwa utaratibu wa kisheria ni vema TFF, wadau wa mpira na jamii kwa jumla kuwa na subira na kuicha dola kufanya kazi yake.
TFF inachukia vitendo vyovyote vinavyosababisha kuvuja kwa mapato yatokanayo na viingilio vya mpira wa miguu na inayo nia ya dhati ya kuhakikisha fedha zinazopatikana kwenye mpira zinausaidia mpira wenyewe.
Katika kutekeleza hilo TFF iliunda Kamati maalumu ambayo pamoja na mambo mengine ni kazi yake ni kukusanya maoni ya wadau ili kubaini na hatimaye kuziba mianya ya upotevu wa fedha zitokanazo na mapato ya viingilio.

Fredrick Mwakalebela
KATIBU MKUU

No comments :

Post a Comment