Mashuja wa simba katika mchezo wa leo walikuwa n Mohammed Banka aliyefunga goli la kwanza na Musa Hassan "Mgosi" aliyefunga goli la pili katika kipindi cha kwanza.
Kipindi cha pili ambacho kilianza kwa kasi huku klabu ya Lengthen Fc ikifanya jitihada za kusaka hata goli moja la kufutia machozi lakini walinzi wa Simba walifanya kazi nzuri ya kuwadhibiti safu ya washabuliaji wa klabu hiyo changa ya Zimbabwe.
MOhammed Kijuso ndiye aliyehitimisha karamu ya magoli 3-0 kwa Simba.
Ushindi huo unaifanya Simba sasa kutengeneza mazingira mazuri ya kusonga mbele, pindi watakapokutana wikki mbili zijazo katika mchezo wa marudiano ambapo Simba sasa itakuwa nyumbani.
Klabu ya Simba inatarajiwa kureje Tanzania Kesho asubuhi kuanza maandalizi ya mchezo wa marudiano.
No comments :
Post a Comment