Klabu ya Liverpool itakutana na klabu ya Ureno, Benfica katka hatua ya robo fainali ya michuano ya Europa League, wakati klabu ya Fulham itakutana na mabingwa watetezi wa ligi kuu ya Ujerumani, Wolfsburg.Liverpool, ambayo ilijikuta ikitua katika mashindano haya baada ya kutolewa katika hatua ya kwanza ya mtoano baada ya kutolewa katika ligi ya mabingwa, walikata tiketi ya kutinga hatua ya robo fainali baada ya kuichapa klabu ya Ufaransa, Lille 3-1 kwa magoli ya Jumla. Liverpool na Benfica wanarekodi ya kushinda mara saba UEFA CUP.
Fulham, ushindi iliyoupata wa magoli 4-1 dhidi ya klabu kongwe ya Serie A, kibibi kizee cha Turin Juventus na kusonga mbele kwa jumla ya magoli 5-4, sasa itakutana na Wolfsburg, timu nyingine ambayo iliondolewa katika hatua ya mtoano ya ligi ya mabingwa.
Robo fainali zingine mbili, Hamburg ambayo uwanja wake ndiyo utakaotumika kwa fainali za mwaka huu, Hamburg Arena, watakutana na Standard Liege ya Ubelgiji, na huku klabu za Hispania zikiuana zenyewe kwa zenyewe yaani Valencia na Atletico Madrid.
Michezo ya kwanza ya robo fainali imepangwa kuanza kupingwa April 1, huku michezo ya marudiano ikipigwa April 8.
Michezo ya nusu fainali itachezwa kati ya April 22 na 29, huku fainali ikipigwa siku ya Jumatano katika uwanja wa Hamburg Arena hapo May 12.
ratiba kamili ya UEFA CUP
Fulham v Wolfsburg
Hamburg v Standard Liege
Valencia v Atletico Madrid
Benfica v Liverpool
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment