Uongozi wa klabu ya Yanga wajikanyaga dhidi ya maamuzi ya taarifa iliyotolewa na kocha Kostadin Bozidar Papic ya kwamba anampango wa kuwamwaga kutokana na kutopata stahili yake ipasavyo.
Luisi Sendeu ni Afisa Habari wa Yanga, amekiri kocha huyo anawadai mshahara wa mwezi mmoja lakini amewataka mashabiki kusubiri makubaliano watakayoyafikia na uongozi wa klabu hiyo yenye maskani yake Jangwani.
Kwa mujibu wa taarifa ambayo imechapipshwa na magazeti leo, Papic amebainisha kwamba amechoshwa na vitendo anavyofanyiwa na Uongozi wa klabu ya Yanga ikiwa ni pamoja na kutompatia malipo yake kwa wakati, jambo ambalo limekuwa likimfanya atumiwe fedha toka Serbia badala ya mshahara ambao anastahili kupata.
Aidha Papic amesema hapewi heshima anayostahili na viongozi wa klabu ya Yanga jambo ambalo anahisi kama wanamdharau na ndiyo maana wanamnyanyasa licha ya kuibadili Yanga na kucheza soka bora.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment