TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
ZAIDI YA MILIONI MOJA WAJIUNGA NA NIPE NIKUPE YA ZAIN
Dar es Salaam Machi 14, 2010
Zaidi ya wateja milioni moja wamejiunga na ofa mpya ya Zain ya Nipe Nikupe iliyozinduliwa Januari 28 Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Zain Tanzania, Khaled Muhtadi.Meneja Uhusiano wa Zain Tanzania Muganyizi Mutta amesema katika taarifa iliyotolewa jijini Dar es Salaam kwamba wateja wa Zain wanotumia ofa ya nipe nikupe ya kwanza ya aina yake Barani Afrika sasa wamefika milioni moja.
“Wateja wetu walikuwa wanataka unafuu wa kuongea na sasa wamepata. Zain inawarudishia wateja walio katika mpango wa Malipo Kabla pesa yote waliyotumia kupiga simu kutoka mtandao wa Zain kwenda mtandao wowote ule nchini siku hiyo hiyo papo papo, siyo kesho, wala kesho kutwa. Ni huduma ya Kipekee Barani Afrika na haina mpinzani,’’ alisema Mutta.
‘’ Tumeweka rekodi ya kuwarudishia mara mbili muda wa maongezi wateja wetu na hii ni kwenda mtandao wowote ule kuwaongezea muda wa kuwasiliana kupitia Nipe Nikupe ofa ya kwanza ya aina yake nchini Tanzania, ” alisema Mutta.
Wateja wa Zain walio katika mpango wa Malipo Kabla nchini kote wanarudishiwa Tsh 200 papo kwa papo kwa kila Tsh 200 wanayoitumia kila siku kupiga simu kutoka mtandao wa Zain kwenda mtandao wowote ule wa simu za mkoni nchini Tanzania ili mteja aendelee kupiga simu kwenda Zain au simu kwenda mtandao mwingine nchini.
“Tungependa wateja wetu wote wa Malipo Kabla wajiunge na Nipe Nikupe ili wanufaike na ofa hii ambayo haina mpinzani nchini Tanzania, ” alisema Mutta na kuongeza kwamba nipe nikupe imeanzishwa kuwazawadia wateja wa Zain kwa uaminifu wao na kwa kuichagua Zain kuwa mtandao wao wa mawasiliano na kuifanya kuwa mtandao Unaoheshimika zaidi Tanzania.
Kujisajili katika nipe nikupe, mteja anatuma SMS neno NIPE mara moja tu kwenda namba 15444, gharama za kujisajili ni ths 500 ambazo zinatozwa mara moja tu mteja anapojiunga. Kuangalia bonasi zake mteja anapiga *102#. Muda wa maongezi wa bonasi unaisha saa sita usiku siku hiyo hiyo.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment