Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, March 6, 2010

SIMBA BADO POINTI MBILI KUTANGAZA UBINGWA

Wekundu wa Msimbazi Simba wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa magoli 3-1 dhidi ya JKT Ruvu katika mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara uliyochezwa katika uwanja w Uhuru.
Simba ndiyo ilikuw aya kwanza kupata goli kupitia kwa mchezaji Mohammed Banka kwa shuti kali kabla ya mchezaji Bruno Adolf wa JKT Ruvu aliyefunga kwa mkwaju wa Penati kabla ya kwenda mapumziko.
KAtika dakika za lala salama Mussa Hassan Mgosi alifunga goli la pili kabla ya mchezaji Uhuru Suleimani kufunga goli la tatu na kuwafanya kuibuka na ushindi wa magoli 3-1.
Hata hivyo mchezaji Mwinyi kazimoto alijikuta akitolewa kwa kadi nyekundu kufuatia kuzozana na mwamuzi jambo ambalo litamfanya mchezaji huyo tegemeo wa JKT Ruvu kukosa michezo mitatu iliyosalia katika ligi kuu Tanzania Bara.
Kufuatia ushindi huo, Simba sasa imefikisha Jumla ya pointi 53 huku wakiwa wamesaliwa na pointi mbili kuweza kutangaza ubingwa.
katika mchezo mwingine uliyochezwa mjini Morogoro Mtibwa Suger imefanikiwa kuifunga timu ya Moro United jumla ya magoli 2-0, na kuwafanya sasa kufikisha jumla ya pointi 30.
Huko Kaitaba, timu ya Kagera Suger imelazimishwa sare ya bila kufungana na klabu ya Afrika Lyon.

No comments :

Post a Comment