Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, March 20, 2010

KAMPUNI YA BUSINESS TIMES "THE BIZE" MABINGWA KOMBE LA NSSF

TIMU ya soka ya Kampuni ya Business Times, 'The Bize' imetawazwa kuwa mabingwa wapya wa michuano ya NSSF Media Cup 2010, baada ya kuichapa Wizara ya Habari Utamaduni na Michezo ya Zanzibar kwa penalti 9-8, katika fainali zilizofanyika katika uwanja wa TCC Chang'ombe, Dar es Salaam.
Ubingwa huo ni zaidi ya ubingwa wa Simba kwani The Bize imetwaa ubingwa huo bila ya kupoteza mchezo hata kutoa sare wakati mabingwa wapya wa Bara wametoka sare michezo miwili.
The Bize hadi wanatinga hatua ya fainali na kutwaa ubingwa huo, waliichapa Radio Kheri mabao 2-0. kabla ya kuitandika NSSF mabao 2-1 na kuishushia kiama IPP mabao 6-0.
Kwa ushindi huo The Bize walijinyakuliwa kitita cha sh. milioni 3 na kikombe walichokabidhiwa na Waziri wa Michezo na Utamaduni George Mkuchika ambaye alikuwa mgeni rasmi katika fainali hiyo.
The Bize waliwainua mashabiki wao dakika ya 17 ya mchezo huo kupitia kwa Martin Peter baada ya kuachia shuti kali akimalizia kazi nzuri iliyofanywa na Dismas Bahatia.
Wakitandaza kandanda safi huku wakigongeana pasi fupi fupi, The Bize waizidisha mashambulizi langoni mwa wapinzani wao ambapo dakika ya 43 walipata bao la pili lililofungwa na George Dennis kwa shuti kali lililomshinda kipa wa Habari Zanzibar Abduhim Juma.
Kipindi cha pili Zanzibar walicharuka na kuanza kulisakama lango la The Bize na dakika ya 60 walipata bao la kwanza lililofungwa na Abduhim Juma kwa njia ya penalti baada ya mabeki kucheza rafu katika eneo la hatari.
Habari Zanzibar walisawazisha bao la pili katika dakika ya 75 kupitia kwa Amour Mussa baada ya mabeki wa The Bize kujichanganya.
Kufuatia matokeo hayo mpaka mwisho wa mchezo zilipigwa penalti ambapo The Bize ambao pia ni wachapishaji wa magazeti ya Majira, Spoti Starehe, Business Times na Dar Leo waliibuka na ubingwa baada ya kuichapa Habari Zanzibar kwa penalti 9-8.
Katika mchezo wa soka The Bize walizawadiwa kombe pamoja na kitita cha sh. milioni 3, wakati nafasi ya pili ilichukuliwa na Habari Zanzibar ambao walipewa kombe na sh. milioni 2 na Mwananchi waliambulia milioni 1.
Katika mchezo wa Netiboli NSSF walishika nafasi ya kwanza baada ya kuichapa Mwananchi kwa mabao 44-12 na walizawadiwa kombe na sh. milioni 2.5, Mwananchi Queens walipata sh. milioni 1.5 wakati The Bize Queens waliambulia sh. 750,000 na wafungaji bora wa netiboli ni Lulu Habibu wa The Bize Queens ambaye ana mabao 65 wakati mfungaji bora kwa upande wa soka ni Majuto Omary wa Mwananchi na wote walipata sh. 200,000 kila mmoja.

No comments :

Post a Comment