Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, March 19, 2010

TWIGA STARS JUMAMOSI KUIVAA ETHIOPIA

Timu ya taifa ya Tanzania ya wanawake Twiga Stars Jumamosi itashuka dimbani kuikabili timu ya taifa ya Ethipia ya wanawake katika mchezo wa kuwani kufuzu kucheza fainali za mataifa ya Afrika zitakazochezwa huko nchini Afrika kusini baadae mwaka huu.
Twiga stars hiyo kesho wanashuka katika dimba la Uhuru jijini Dar es salaam huku wakichagizwa na kumbu kumbu ya ushindi wa mabao matatu kwa moja walioupata dhidi ya wapinzani wao katika mchezo wa kwanza uliounguruma majuma yaliyopita huko mjini Adis Ababa nchini Ethiopia.
Akiuzungumzia mchezo huo wa Jumamosi raisi wa chama cha soka la wanawake nchini Lina Madina Muhando amesema mchezo huo utakua mgumu kwa pande zote mbili lakini shilingi ya ushindi akaiangushia kwa Twiga Stars.
Lina Madina Muhando pia amewataka watanzia kwa ujumla hususana kina mama kujitokeza kwa wingi kwenye uwanja wa uhuru hapo kesho.
Katika kuhakikisha wimbi la ushindi linaendelezwa katika mchezo huo wa Jumamosi kampuni ya bia ya Serengeti imetoa msaada wa shilingi milion 4.5 kama msaada ambao umekua ukihitajika kwa hali na mali katika timu hiyo ya wanawake.
Msaada huo wa kampuni ya bia ya Serengeti umewasilishwa TFF hii leo na Afisa Uhusina na mawasiliano wa kampuni hiyo Teddy Mapunda ambae pia amewataka watanzani kujitokeza uwanjani kwa wingi hiyo kesho kuishangilia Twiga Stars.
Nayo kampuni ya CXC HOLDING kupitia kwa mkurugenzi wake Charles Hamka nayo imekabidhi hundi ya shilingi milion kumi kwa lengo la kuisaidia timu hiyo.
Wakati misaada hiyo ikitolewa kwa lengo la kuisaidia timu ya Twiga Stars, kocha mkuu wa timu hiyo Charles Boniphas Mkwasa amesema kikosi chake kitaingia uwanjani kwa lengo la kuendeleza mazuri waliyokwisha yaanza huko nchini Ethiopia majuma mawili yaliyopita.
Kwa upande wake nahodha wa Twiga Stas Sophia Mwasikili nae amewaahidi ushindi watanzani kwa ujumla huku akiweka bayana malengo yao mwaka huu ni kucheza fainali za mataifa ya Afrika huko nchini Afrika kusini.

No comments :

Post a Comment