Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, March 25, 2010

WAPINZANI WA TAIFA STARS - SOMALIA WAWASILI


Timu ya Taifa ya Somalia The Ocean Starz imetua leo tayari kwa mchezo wake wa Jumamosi dhidi ya Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Starz kwenye mchezo wa kuwania kufuzu fainali za mataifa bingwa barani Africa CHAN utakaopigwa kwenye uwanja wa UHURU.

The Ocean Starz imetua ikiwa na msafara wa watu 25 huku ikiwa na matumaini makubwa ya kuishinda Starz hapo Jumamosi.

Nahodha wa kikosi hicho Yusuph Ali Nur amesema mchezo huo utakuwa mgumu lakini wamejiandaa vyema kuhakikisha wanaibuka na ushindi.

Msafara uliowasili leo ni pamoja na viongozi Abdikani Said Arab,Basher Mohamed Gesey,Yaxye Maxamed Abukar,Mohamed Abdulle Farayare na Abdulkadir Abdirahman Ali.

Wachezaji ni pamoja na Dahir Mohamud Mukhtar,Wa’di Kassim Hassan,Mohamed Abdullahi Aboki,Osman Yusuf Osman,Tahlil Mohamed Mohamud,Hassan ahmed Mohamed,Hassan Ali Roble na Kamal Ali Omar.

Wengine ni Nahodha Yusuf Ali Nur,Mohamed Hashi Siyad,Mohamed Hassan Ali,Abdifitah Abdi Osman,Badri Moallin Ahmed na Jabril Hassan Mohamed.

Ndani ya kikosi hicho pia wamo Mahad Mohamed Haji,Aadan Hussein Ibrahim,Mustaf Hassan Mohamed,Anwar Sadad Ibrahim,Sidi Said Abdulla na Mohamed Yare Isak.

Wakati huo huo Benki ya NMB leo wamekabidhi kiasi cha shilingi milioni 21 kwa Taifa Starz ikiwa ni maandalizi kwa mchezo huo wa Jumamosi dhidi ya Somalia The Ocean Starz.

Mbali na fedha hizo Starz imekabidhiwa vifaa mbalimbali vya michezo vikiwemo jezi,vizuia ugoko(Shin Guard),viatu,soksi na bips vyote vikiwa na thamani ya kiasi cha shilingi milioni 15.

Mkuu wa Masoko wa benki ya NMB IMANI KAJULA amesema wametoa vifaa hivyo kutambua umuhimu wa mchezo huo wa Jumamosi.


Naye Katibu Mkuu wa shirikisho la soka nchini TFF FREDRICK MWAKALEBELA amesema maandalizi kiutawala tayari yamekamilika na vifaa hivyo vitasaidia pia kwa mchezo dhidi ya Rwanda Amavubi kama watafanikiwa kuwaondoa The Ocean Starz Somalia.

No comments :

Post a Comment