Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, October 15, 2013

MISS TANZANIA 2012, BRGITTE ALFRED AFANYIWA BONGE LA PATI


 Redds Miss Tanzania 2012 ambaye pia ni Miss Sinza 2012, Brigitte Alfred (wa kwanza kushoto) akiwa katika pica ya pamoja na Mkurugenzi wa Lino International Agency, Hashim Lundenga (wa pili kulia), Miss Tanzania wa sasa Happiness Watimanywa na Mama wa Brigitte Veridiana Mashingia wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa sherehe ya kupongeza (Brigitte) kwa kushinda nafasi ya tatu ya taji la dunia la kipingele cha urembo wenye malengo maalum. Mrembo huyo aliwashinda warembo 127.Sherehe hiyo ilifanyika kwenye hotel ya Giraffe Ocean mwishoni mwa wiki.

Mwandishi wetu
Redds Miss Tanzania 2012, Brigitte Alfred Lyimo amesema kuwa ushindi wake wa nafasi ya tatu katika kipengele cha urembo wenye malengo maalum katika mashindano ya Miss World mwaka huu ni wa  Watanzania wote.
Brigitte alisema hayo katika hafla ya kuagwa iliyoandaliwa na waandaaji wa mashindano ya urembo nchini, kampuni ya Lino International Agency iliyofanyika kwenye hotel ya Giraffe.
Alisema kuwa amefarijika sana kushinda nafasi hiyo kwani ilishirikisha warembo wote walioshindana mwaka huu katika mashindano hayo. Alisema kuwa hakuwa kazi rahis kushika nafasi hiyo kwani kipengele hicho ushirikisha warembo wote.
“Namshukuru mama yangu,  Verdiana Mashingia ambaye alikuwa bega kwa began a mimi katika kuhakikisha mradi wangu wa ujenzi wa bweni la albino wa shule ya smingi Buhangija shinyanga unafanikiwa, pongezi pia kwa kamati ya Miss Tanzania na wadhamini, Redds,” alisema Brigitte.
"Ndoto zangu za kuitumikia jamii hazitaishia hapa, nitaitumikia na nitaendelea kuwasaidia Albino ambao wamenichagua kuwa barozi wao," alisema mrembo huyo.
Aidha Brigitte alimpongeza Hapiness na kumtaka atumie kipaji alichonacho na urembo wake wa asili kuitoa kimasomaso Tanzania kwenye mashindano ya mwakani.
Mkurugenzi wa Lino International Agency, Hashim “Uncle” Lundenga alisema kuwa Brigitte amefanya kitu cha kihistoria Tanzania na kuzishinda nchi kubwa mbali mbali kama Uingereza, Ufaransa na nyingine nyingi.
Lundenga alisema kuwa wamefarijika kwa mafanikio hayo na ndiyo maana wameamua kufanya hafla hiyo ambayo ni ya kihistoria huku akiwapongeza wadhamini, Redds kwa kudhamini hafla hiyo.
Alisema kuwa ni vigumu kuamini, lakini ukweli unabaki pale pale kuwa fai yao inazidi kukuwa, tena kwa mafanikio tofauti na watu wanavyodhani.
“Mfano mzuri ni mama yake Brigitte alivyokuwa bega kwa bega wakati wote mwanaye alivyokuwa na taji, huu ni mfano wa kuigwa na tunaomba wazazi wafuate nyayo za mama huyu,” alisema Lundenga.
Lundenga alisema kuwa Brigitte ameleta changamoto kubwa kwa mrembo wa sasa Happiness Watimanywa katika mashindano yanayofuata ya urembo ya dunia.
"Brigitte amefanya vizuri japo hakufanikiwa kutwaa taji la dunia, kuwa namba tatu kwenye taji la mrembo mwenye malengo ambalo kuacha taji la dunia ili linafuatia, Brigitte anahitaji kupongezwa," alisema.
Alisema kuwa Brigitte ameonyesha ushujaa na kuwapita warembo kutoka mataifa makubwa dunia ambao walichuana kwenye mashindano hayo na yeye kufanikiwa kuingia hatua ya tatu bora kwenye taji hilo.

No comments :

Post a Comment