Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, October 27, 2013

WAANDISHI WA HABARI WAPIGWA 'STOP' KURIPOTI UCHAGUZI WA TFF




Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) Juma Pinto (katikati) akizungumza na Waandishi wa Habari nje ya Ukumbi wa Mikutano NSSF  'Water Front', mahala unapofanyika Uchaguzi mkuu wa Rais na viongozi wa Soka wa Shirikisho la mpira wa miguu nchini (TFF).

KATIKA hali isiyo ya kawaida, Waandishi wa Habari  wamezuiwa kuripoti habari za uchaguzi mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), uliofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa NSSF Water Front.
Baada ya waandishi kuzuiwa, askari waliokuwa wakilinda usalama katika uchaguzi huo waliwataka waandishi kuondoka na kukaa mbali na ukumbi huo huku  Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo (TASWA), Juma Pinto, akiwataka waandishi kususia kuandika na kuripoti matokeo ya uchaguzi huo ikiwa ni pamoja na kutoandika taarifa za TFF.
Pinto alisema kitendo cha TFF kupitia kwa Mwenyekiti wa Kamati ya uchaguzi, Hamidu Mbwezeleni, kuwazuia waandishi kuripoti habari hizo ni cha udhalilishaji kwa kuwa waandishi ndio waliokuwa mstari wa mbele kuandika taarifa za uchaguzi huo tangu mchakato wake ulipoanza Februari mwaka huu.
Alisema mbali na kutoruhusiwa kuripoti uchaguzi huo, Mbwezeleni ametoa kauli ambazo si za kiungwana na kusahau kuwa waandishi ndio waliokuwa mstari wa mbele kuwajuza Watanzania kuhusu uchaguzi huo kwa faida ya maendeleo ya soka la Tanzania.

 Kufuatia hali hiyo, iliwalazimu waandishi kukaa nje ya ukumbi huku wakiuliza kwa wajumbe kitu gani kinachoendelea ndani ya ukumbi.

No comments :

Post a Comment