Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, June 26, 2012

MASHALI SASA AWATAKA CHEKA, KASEBA




Mashali akivalishwa mkanda wake wa ubingwa baada ya kuutetea jana kwa kumtwanga TKO raundi ya tano Maisha


Na Prince Akbar
BAADA ya kumtwanga kwa Technical Knockout (TKO) raundi ya tano Samson Maisha wa Mbeya, bingwa wa Taifa wa TPBO, Thomas Mashali 'Simba wa Teranga' amesema anamtaka mshindi wa pambano kati ya Japhet Kaseba na Francis Cheka apande naye ulingoni, ili adhihirishe yeye ndiye ‘king’ wa ndondi Tanzania.
Mashali akiwa amemdondosha Maisha jana
Akizungumza na BIN ZUBEIRY kwenye ukumbi wa Friends Corner, Manzese jana baada ya ushindi wake huo, Mashali alisema kwamba anaamini kwa sasa katika nchi hii hana mpinzani na ameomba yeyote atakayeshinda kati ya Kaseba na Cheka asikwepe kupanda naye ulingoni.
“Huyu mtoto (Maisha), si saizi yangu, wamempakazia tu, baada ya kuona mabondia wote wa Dar es Salaam sasa hivi wananiogopa, nilikuwa nampiga huku namhurumia, na bado amefia katikati ya safari (raundi ya tano). Namtaka mshindi kati ya Kaseba na Cheka,”alisema Mashali.  
Katika pambano hilo la jana la uzito wa Middle, Mashali alimzidi uwezo mpinzani wake kuanzia raundi ya kwanza na katika raundi ya tano alimkalisha chini kwa ngumi kali ya mkono wa kulia.
Maisha alijitutumua kuinuka ili aendelee na pambano, lakini alionekana dhahiri hajiwezi na ndipo Kocha wake, Bagaza Mambane akarusha taulo ulingoni. Hata hivyo, Maisha anaonekana ni bondia mzuri akipata mazoezi zaidi na ujanja wa katika masumbwi. 

No comments :

Post a Comment