Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, June 28, 2012

SAFARI LAGER YATANGAZA KUDHAMINI MASHINDANO YA TANZANIA INTERNATIONALOPEN DARTS CHAMPIONSHIPS JIJINI MWANZA.



  Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu udhamini wa mashindano ya Darts yanayojulikana kwa “Tanzania International Open Darts Championships” yanayotarajiwa kuanza kesho jijini Mwanza.Kulia ni Mwenyekiti wa Chama cha Darts Taifa, Gesase Waigama.

  Mwenyekiti wa Chama cha Darts Taifa, Gesase Waigama (kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu udhamini wa Safari Lager kwenye mashindano ya Darts yanayojulikana kwa “Tanzania International Open Darts Championships” yanayotarajiwa kuanza kesho jijini Mwanza.Kulia ni Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo
KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager leo imetangaza rasmi kudhamini mashindano ya Kimataifa ya mchezo wa Darts yatakayojulikana kwa “Tanzania International Open Darts Championships” ambayo yanatarajiwa kuanza rasmi kesho Ijumaa Julai 01,2012 jijini Mwanza .
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam leo, meneja wa bia ya Safari Lager Bw. Oscar Shelukindo amesema Safari Lager imesaidia kiasi cha MILIONI 32 za kuendesha mashindano hayo ikiwa ni pamoja na zawadi za vikombe na pesa taslimu.“Safari Lager inaendeleza lengo lake la kusaidia kukuza zaidi mchezo wa Darts hapa Tanzania.Alisema Bw. Shelukindo. Safari Lager imekuwa ikidhamini mashindano mbalimbali ya mchezo wa Darts, na imegawa pia vifaa vya michezo kwa maeneo mbalimbali ya kuchezea Darts Dar Es Salaam na mikoani.
Naye mwenyekiti wa Taifa wa chama cha Darts cha Taifa (TADA) Bw. Gesase N. Waigama, ambaye pia ni raisi wa shirikisho la Darts Afrika Mashariki alisema timu shiriki katika mashindano haya ni Kenya,Uganda,Tanzania na Rwanda.
Gesase alisema mtindo utakaotumika katika mchezo huo ni wa Kitaifa kwa kushirikisha timu ya taifa ya kila nchi,Vilabu,Doudles na Singles.
Mashindano hayo yataanza kesho katika Hotel ya Monac Kirumba na yanatarajiwa kufikia tamati jumapili Julai 3,2012 jijini Mwanza
You might also like:

No comments :

Post a Comment