Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, September 22, 2012

‘APATE RAHA’ YA SUMA LEE HIYOOO RUNINGANI




Na Elizabeth John
NYOTA wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ismail Seif  ‘Suma Lee’ ameachia video ya wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la ‘Apate raha’ ambao unafanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Suma Lee alisema video ya wimbo huo imeanza kuonekana hivi karibuni na ana uhakika utafanya vizuri kutokana na mandhari aliyotumia katika kuitengeza video hiyo.
“Namshukuru Mungu kazi zangu huwa zinapokelewa vizuri na mashabiki wangu, kitu ambacho kinanipa morali ya kuendelea kufanya kazi,” alisema Suma Lee.
Suma Lee akawaomba mashabiki wake waendelee kumpa sapoti katika kazi zake na kwamba wasicheze mbali na yeye kuna vitu vingi vizuri ambavyo amewaandalia.
Ukiondoa kibao kipya cha Apate raha, Suma Lee aanaendelea kukumbukwa kwa vibao vyake vingine kama, Chungwa, Hakunaga, Asiyecheza atoke na nyinginezo ambazo zilimtambulisha na kufanya vizuri katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya nchini kwa nyakati tofauti.

No comments :

Post a Comment