Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, September 20, 2012

ZAWADI SAFARI POOL TAIFA 2012 ZATANGAZWA




Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo akizungumza na waandishi wa habari
Na Elizabeth John
KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager, leo imetangaza zawadi za washindi wa mashindano ya Safari Pool Taifa yanayotarajiwa kufanyika Septemba 26 hadi 29, mwaka huu jijini Mwanza kwa kushirikisha mabingwa wa klabu kutoka mikoa 16 ya Tanzania.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo alisema zawadi kwa bingwa wa fainali za Safari Pool Taifa 2012 ni pesa taslimu shilingi milioni tano, Kombe na Medali za dhahabu kwa washindi wa upande wa timu.
Shelukindo alisema kuwa, zawadi za washindi wa pili itakuwa ni shilingi 2,500,000, huku washindi wa tatu wakiondoka na kitita cha shilingi 1,250,000, ambapo washindi wa nne watajinyakulia shilingi 750,000.
Alisema kwa upande wa mchezaji mmoja mmoja, mshindi kwa wanaume atajinyakulia kiasi cha shilingi 500,000, huku bingwa wa wanawake akinyakua shilingi 350,000 na mshindi wa pili wanaume atapata shilingi 250,000.
Mshindi wa pili kwa wanawake, ataondoka na shilingi 200,000 na mshindi wa tatu kwa wanaume atapata shilingi 200,000, huku mshindi wa nafasi hiyo kwa wanawake akiondoka na kitita cha shilingi 150,000.
Katibu wa Chama cha Pool Taifa (TAPA), Amos Kafwinga, alizitaja klabu zilizofuzu kushiriki fainali za Taifa jijini Mwanza kuwa ni Balele ya Tanga, Mbosho ya Kilimanjaro,  2 Eyes ya Arusha, Janja Wild ya Manyara, Sabasaba ya Lindi na Texas ya Tabora.
Nyingine ni New Stand ya Shinyanga, Anatory ya Morogoro, Atlantic ya Dodoma, Nginja ya Iringa, Blue House ya Mbeya, Sun City ya Temeke, Kayumba ya Ilala, Meeda kutoka Kinondoni, huku wenyeji wa mashindano hayo Mwanza wakitarajiwa kuwakilishwa na klabu ya Paseansi.

No comments :

Post a Comment