Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, September 24, 2012

BENKI YA KCB TANZANIA YATOA MSAADA WA VIFAA HOSPITALI YA TEMEKE




 Matroni wa Haopitali ya Temeke jijini Dar es Salaam, akitoa ukaribisho kwa wageni mbalimbali waliofika katika hafla ya kupokea msaada wa vifaa mbalimbali vya Hospitali ya Temeke na Buguruni Vilivyotolewa na Benki ya KCB Tanzania vikiwa na thaman ya shilingi milioni 17,152,000.
 Mkurugenzi wa Bodi wa Benki ya KCB Tanzania Mama Zuhura Muro,(kulia) akimkabidhi Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Temeke jijini Dar es Salaam, DR.Amani Malima,mashine ya kumsaidia mgonjwa kupumulia wakati wa hafla ya kukabidhiwa vitu mbalimbali kwa ajiri ya Hospitali ya Temeke na Buguruni vyenye thamani ya shilingi Milioni 17.152.000.(katikati) Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Temeke James Magoti.
 Mkurugenzi wa Bodi wa Benki ya KCB Tanzania Mama Zuhura Muro,(kulia) akimkabidhi Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Temeke jijini Dar es Salaam, DR.Amani Malima,akimkabidhi msaada wa Folding Screens moja kati ya 3 zilizotolewa msaada na benki hiyo ikiwemo vitu mbalimbali vyenye thamani ya shilingi milioni 11,152,000 ka ajiri ya hospitali hiyo. (Kulia) Mwenyekiti wa Bodi ya Hospitali ya Temeke James Magoti.
Wafanyakazi wa benki ya KCB Tanzania wakiongozwa na Mkurugenzi wa Bodi wa Benki ya KCB Tanzania Mama Zuhura Muro, wakiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Hospitali ya Temeke na Buguruni zote za jijini Dar es Salaam, baada ya KCB kukabidhi Msaada wa vifaa mbalimbali kwa hospitali hizo wenye thamani ya shilingi Milioni 17,152,000.

Na Mwandishi wetu
Benki ya KCB Tanzania, imetoa msaada wa vifaa mbalimbali kwa ajili ya kusaidia afya ya mama na mtoto vyenye thamani ya shilingi 17,152,000/- kwa hospitali za Temeke na Buguruni zilizopo jijini Dar es Salaam
Akizungumza katika hafla fupi ya makabidhiano ya vifaa hivyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, mkurugenzi wa bodi ya benki hiyo Zuhura Muro alisema katika kuhadhimisha wiki ya jamii mwaka huu benki ya KCB imeamua kuelekeza misaada yake katika sekta ya afya
“Wakati wa wiki ya jamii mwaka jana na juzi tulitoa madawati na vitabu kwa shule mbalimbali nchini. Mwaka huu tumechagua kusaidia sekta ya afya hasa kwa upande wa akinamama na watoto ili kupunguza idadi ya vifo vitokanavyo na uhaba wa vifaa muhimu hospitalini,”
“Mkurugenzi huyo wa bodi alisema benki ya KCB inaatambua umuhimu wa afya ya mama na mtoto na ndiyo maana tumeona ni jambo zuri kuwekeza katika sekta ya afya. Nikiwa kama mama ninayo furaha kwa kuwa naamini msaada huu utaweza kuokoa maisha ya akina mama na watoto,” alieleza
Kwa upande wake mganga mfawidhi wa hospitali ya Temeke Amani Malima alisema kuwa hospitali yake imekuwa ikihudumia akina mama wengi kuliko uwezo wake kutokana ukosefu wa vifaa.
“Tunapokea akina mama wengi wanaokuja kujifungua zaidi ya uwezo wetu. Wengine huwa wanazaliwa wakiwa bado hawajatimia na hulazimika kuwapa rufaa ya kwenda hospitali nyingine kama Muhimbili kutokana na kutokuwa na vifaa. Tunaishukuru benki ya KCB kwani msaada huu utasaidia kuboresha hali,” alisema
Naye mganga mfawidhi wa hospitali ya Buguruni Dr Hawa Lesso aliishukuru benki ya KCB na kusema kuwa utasaidia kuokoa maisha ya watoto wanaozaliwa kabla wakiwa hawajatimia (pre mature).
Watoto wanaozaliwa kabla ya kutimia wakati mwingine hupoteza maisha kabla ya kuwapa rufaa ya kwenda hospitali nyingine kutokana na ukosefu wa vifaa. Tunaishuru benki ya KCB kwani imesikiliza kilio chetu, Tunaomba taasisi nyingine za kifedha kuiga mfanio wa benki ya KCB.
Vifaa vilivyotolewa kwa hospitali ya Temeke ni pamoja na mashine moja ya joto kwa watoto waliozaliwa bila kutimia (Incubator), Folding screens 10, seti ya mashine ya hewa 3 (Oxygen flow meter) na sare za wauguzi pea 10 vyote vikiwa na thamani ya shilingi 11,252,00/-
Hospitali ya Buguruni ilipokea mashine moja ya joto kwa watoto waliozaliwa bila kutimia yenye thamani ya shilingi 5,900,000/-

No comments :

Post a Comment