Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, September 25, 2012

TANZIA; MWANDISHI TANZANIA DAIMA AFARIKI DUNIA LEO






DAR ES SALAAM, Tanzania
MWANDISHI wa habari wa Kampuni ya Free Media Ltd inayochapisha magazeti ya Tanzania Daima na Sayari, Agnes Yamo, amefariki dunia alfajiri ya leo kwenye Hospitali ya Jeshi Lugalo jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Habari Mseto, Mhariri Mtendaji wa Tanzania Daima, Absalom Kibanda, amesema familia ya marehemu Agnes imethibitisha kutokea kwa msiba huo na kuwa marehemu amekufa wakati akipata matibabu kutokana na upungufu wa damu.
Kibanda ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini (TEF), aliongeza kuwa msiba wa Agnes uko nyumbani kwa kaka yake Buguruni Sokoni (Rozana) kwenye mafleti ya Muhimbili.
Enzi za uhai wake, Agnes aliyezaliwa Agosti 9, 1978, alikuwa mwandishi aliyefanya kazi Kampuni ya Habari Corporation, kabla ya Tanzania Daima alikofanya uandishi kwa muda na baadaye kugeukia Idara ya Matangazo ya Free Media Ltd inayochapisha gazeti hilo, hadi umauti ulipomkuta.
Kwa mujibu wa Kibanda, mipango ya mazishi inaendelea kufanyika nyumbani kwa kaka wa marehemu, ambapo mwili unatarajiwa kusafirishwa kesho Jumatano jioni kwenda Morogoro yatakakofanyika maziko yake.
Shughuli za kutoa heshima za mwisho na kuuaga mwili wa marehemu zinatarajiwa kufanyika nyumbani hapo kwa kaka yake Buguruni, kabla ya kusafirishwa. Mungu ailaze ROHO ya marehemu mahali pema PEPONI. Ameeeeeen

No comments :

Post a Comment