Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, September 15, 2012

NABISHA AIPELEKA RUNINGANI VIDEO YAKE YA NAJUA



Na Elizabeth John

MWANADADA anayetamba katika tasnia ya muziki wa kizazi kipya nchini, Beatrice Mathew ‘Nabisha’ (pichani) anajipanga kuachia video ya kazi yake inayokwenda kwa jina la ‘Najua’ ambayo inafanya vizuri katika vituo mbalimbali vya redio kwa sasa.

Akizungumza na Habari Mseto jijini Dar es Salaam jana, Nabisha alisema katika wimbo huo amemshirikisha mkali wa muziki huo ambaye anamkubali sana kupitia kazi zake, Banana Zorro.

“Banana ni msanii ninayemkubali sana na nilikua na ndoto za kuimba naye tangu nikiwa mdogo namshukuru Mungu nimetimiza ndoto zangu, naamni kazi hii itafanya vizuri zaidi kutokana na uwepo wake,” alisema Nabisha.

Nabisha alisema, yupo katika michakato ya kuachia albamu yake ya kwanza itakayokuwa na nyimbo nane, ambayo bado hajaipatia jina kutokana ubora wa nyimbo ambazo zitapamba albamu hiyo.

Mbali na Najua, Nabisha alishawahi kutamba na nyimbo zake kama, Kidole gumba, Mapenzi ya kweli na nyinginezo ambazo zilimtangaza na kufanya vizuri katika tasnia ya muziki huo.

No comments :

Post a Comment