Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, September 24, 2012

BARNABA: 'SIJUTII KWA ALIYEKUWA NAYE' INAKUJA KUWASHIKA




Na Elizabeth John
MSANII wa muziki wa Kizazi Kipya nchini, Barnabas Elias ‘Barnaba,’ anajiandaa kuachia 'pini' jipya aliyoipa jina la 'Sijutii kwa niliye kuwa naye.'
Akizungumza na Habari Mseto jijini Dar es Salaam leo, Barnaba alisema yupo katika hatua za mwisho za uandaaji wa song hilo ambalo anaamini litafanya vizuri kutokana uwezo alionao katika tasnia ya muziki.
“Kama kawaida yangu nyimbo zangu nyingi huwa haziwachukizi mashabiki, ni jambo ambalo namshukuru Mungu, kwani ni wasanii wachache ambao nyimbo zao zinafanya vizuri mtaani kiasi hicho,” alisema.
Barnaba alisema anaamini 'Sijutii kwaniliye kuwa naye' kitafuata nyayoz ya vibao vyake vilivyotangualia, na kwamba kwa sasa yupo katika mchakato wa kutafuta mrembo ambae atapamba video ya kazi hiyo.
Mkali huyo amewaomba mashabiki wa muziki nchini kukaa mkao wa kula kukipokea kibao hicho.
Mbali na kibao hicho, Barnaba aanakumbukwa kwa makali yake aliyoyaonesha katika vibao vyake kama, Magubegube, Wrong number, Tulizana, Milele Daima na nyinginezo ambazo zinafanya vizuri katika tasnia ya muziki wa Kizazi Kipya nchini.

No comments :

Post a Comment