Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, September 1, 2013

DIAMOND AMZAWADIA GARI GURUMO





HABARI/PICHA NA EVANCE NG'INGO
MSANII wa muziki wa kizazi kipya Nasib Abdul, Diamond  jana  alimkabidhi gari mwanamuziki mkongwe wa muziki wa dansi nchini aliyestaafu muziki hivi karibuni, Muhidin Gurumo.

Diamond alimkabidhi mzee huyo gari hilo wakati wa hafla ya kuzindua video ya wimbo wake mpya uitwao My Number One iliyofanyika kwenye hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
 Baada ya kuizungumzia video yake hiyo na changamoto aliyokutana nazo wakati wa kutengeneza video hiyo na ndipo alipomuita stejini mzee Gurumo na kuweka wazi  namna ambavyo amekuwa akimpenda na kumheshimu nguli huyo huku akisisitiza kuwa amesikitishwa na namna mzee huyo anavyohangaika kwa sasa.
Ndipo Diamond alipomuita jukwaani na kumkabidhi funguo wa gari hali iliyopelekea wageni waalikwa kupiga kelele za kushangilia baada ya kuguswa na tukio hilo.

Baada ya zoezi hilo, Diamond alimshika mkono mzee huyo na kisha wakiongozana na wageni waalikwa kwa pamoja walitoka nje na kwenda kuliangalia gari hilo kabla ya kurejea ndani na kuendelea na ratiba kama kawaida.
Akizungumzia Video yake hiyo alisema kuwa imemgharimu zaidi ya milioni 50 ambapo aliitengenezea nchini Afrika Kusini.
Ni Video nzuri na ya aina yake ambayo imegusa mazingira halisi ya maisha ambayo alikuwa akiyaimba katika wimbo wake huo wa mapenzi.

No comments :

Post a Comment