Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Sunday, September 15, 2013

WASHIRIKI WA MISS TANZANIA WATEMBELEA KAMPUNI YA TANZANIA DISTILLERIES LIMITED 'KONYAGI'


Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi' David Mgwassa akizungumza na waandishi wa habari baada ya warembo wanaowania taji la Miss Tanzania kufanya zihara katika Kampuni hiyo mwishoni juzi ambayo imedhamini mashindano hayo kupitia kinywaji chake cha Zanzi  .Picha na mpiga picha wetu
Baahi ya Warembo wanaowania taji la Miss Tanzania wakichukua chakula wakati walipotembelea Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi' juzi   ambao ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu
Baahi ya Warembo wanaowania taji la Miss Tanzania wakiwa kwenye pozi wakati walipotembelea Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi'  juzi  Konyagi  ambao ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu
Meneja masoko  ya ndani na nje wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi' ,Vimal Vaghmaria kushoto na meneja masoko wa ksampuni hiyo Joseph Chibhee wakigonganisha grass na Warembo wanaowania taji la Miss Tanzania walipotembelea kiwandani  juzi Konyagi ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu
Meneja masoko  ya ndani na nje wa Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi' ,Vimal Vaghmariakatikati akiwa katika pozi na baadi ya washiriki wa mashindano ya urembo ya Miss Tanzania walipotembelea kiwandani  juzi konyagi  ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu
 Warembo wanaowania taji la Miss Tanzania wakiwa kwenye pozi wakati walipotembelea Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi'  juzi konyagi ambao ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu

Baahi ya Warembo wanaowania taji la Miss Tanzania wakipata chakula wakati walipotembelea Kampuni ya Tanzania Distilleries Limited 'konyagi'    ambao ni wadhamini kupitia kinywaji cha Zanzi Picha na Mpiga picha wetu
NA MWANDISHI WETU

WAREMBO wanaowania taji la Miss Tanzania wametakiwa kupenda na kuthamini bidhaa zinazozalishwa na viwanda vya ndani.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi mkuu wa Kiwanda cha Tanzania Distilleries (KONYAGI) Bw. David Mgwassa wakati akiongea na Warembo 30 wanaowani taji la Miss Tanzania walipotembelea kiwanda hicho jijini Dar es salaam.

"Nyinyi ni mabalozi wazuri wa kutangaza bidhaa za humu ndani  hivyo nawaomba sana mzipende na kuthamini sana bidhaa zote zinazozalishwa na viwanda vya ndani" alisema Bw. Mgwassa.

Amesema kuwa TDL kupitia kinywaji cha Zanzi imeamua kudhamini shindano la Miss Tanzania kwa kiasi cha Milioni 40 ikiwa na lengo la kutangaza kinywaji hicho na pia kuboresha shindano hilo.

Kwa mujibu wa Bw. Mgwassa shindano la Miss Tanzania ni kielelezo muhimu kwa taifa hili na kuwataka warembo hao kutangaza milima kilimanjaro na pia kuitangaza Zanzi kuwa ni bidhaa bora kwa Watanzania kwa lengo la kuinua uchumi wa nchi.

"Nyinyi warembo naombeni sana  Zanzi iwe kwenye mawazo yenu kila siku na muitangaze Zanzi baada ya mlima kilimanjaro kwa kufanya hivyo basi uchumi wa nchiu pia utakua mzuri zaidi." alisema

Kwa upande wake meneja masoko wa TDL, Bw. Vimal Vaghmaria aliwataka warembo hao kuwa na nidhamu kubwa wanapokuwa kambini kwa lengo la kupata mrembo mwenye viwango vya juu na kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya kimataifa.

"Sisi kama TDL kupitia kinywaji cha Zanzi tumemua kudhamini shindano hili la Miss Tanzania tukiamini kuwa nyinyi ni mabalozi wazuri wa kuitangaza kinywaji hichi na kuiletea sifa Tanzania" alisema Bw. Vaghmaria.

Katika ziara hiyo warembo walipata nafasi ya kujione shughuli mbalimbali za kiwanda hicho kuanzia mwanzo wa vinywaji vinapozalishwa hadi kwenye sehemu ya mwisho ya upakiaji.

No comments :

Post a Comment