Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, September 17, 2013

FLOYD MAYWEATHER SASA KUZIPIGA NA AMIR KHAN





BAADA ya kumchakaza Canelo Alvarez, bondia Floyd Mayweather ‘Cash Money’ anamtaka bondia wa England, Amir Khan katika mpambano unaofuata.
Kituo kinachoonyesha mapambano ya ngumi ya Mayweather cha Showtime Sports kimetoa taarifa kuwa kuna uwezekano wa bondia huyo kupambana na Khan ambaye anayatajia kutetea taji lake la IBF uzito wa welter na Devon Alexander mwezi Desemba mwaka huu jijini New York.
Mapambano mawili kati ya sita ya Mayweather yataonyeshwa moja kwa moja kupitia kituo hicho na Mkurugenzi wa Showtime Sports, Stephen Espinoza alisema kuwa wanapenda kuona mpambano huo unafanyika.
Mkurugenzi huyo amepoendekeza mpambano huo unaweza kufanyika Uingereza. "Amir Khan ni mpinzani mzuri wa Floyd Mayweather, kwa sababu ana kasi ulingoni," alisema Espinoza.
"Mpambano huo wa kuvutia unaweza kufanyika Uingereza au New York. Floyd amezungumzia uwezekano wa kufanyika kwa mpambano huo sehemu moja kati ya hizo mbili.
Kama Khan akikubali kupambana na Mayweather, analipwa fedha nyingi sana ambazo anaweza kuwa hajawahi kupata katika maisha yake ya ngumi.
Alvarez alipata pauni 7.9 milioni poamoja na kupoteza mpambano huo. Espinoza alisema kwamba Khan anaweza kuwaongezea soko kubwa katika mpambano huo kuliko ilivyokuwa kwa Alvarez.

No comments :

Post a Comment