Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, August 30, 2011

MABONDIA WA ZAMANI WATAKIWA KUFADHILI NGUMI





BINGWA wa Mchezo wa kick Boxing nchini Japhet Kaseba amewaomba Mabondia wakubwa kuhakikisha wanaweka na kuchangia fedha zitakazo kuwa zikitolewa kuchangia vyama vya michezo nchini wikiwemo RT na BFT.

Akizungumza na Mwandishi wa gazeti hili leo kwa njia ya simu Gwiji huyo wa Mapigano amesema itakuwa ni jambo zuri kwa mabondia wakubwa kutenga fedha ili kuchangia vyama vya michezo mbali mbali nchini wikiwemo vya Ngumi za ridhaa na riadha badala ya kutegemea nguvu ya serikali tu.

"Sifikili kama tukijaribu tutashindwa japo kwa kiasi kidogo kidogo tuweke mazoea ya kuchangia vyama hivi kwa maendeleo ya Taifa kwa ujumla kuliko kutegemea serikali tu"alisema Kaseba.

Hata hivyo Kaseba amesema kuwa baada ya kumalizika kwa mashindano ya All African Games ambayo yanatarajia kurindima hivi karibuni nchini Msumbiji yupo mbioni kuandaa filamu itakayo kuwa ikielezea umuhimu wa kuwekeza katika michezo.

"Lengo la hii filamu ni kujaribu kuwapa hamasa wadau kuwekeza na kuchangia michezo ila pia nataka kuwashirikisha wanamichezo mbali mbali"alisema Kaseba.

No comments :

Post a Comment