Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, August 30, 2011

TTCL YAENDELEA KUTOA MSAADA ZAIDI KWA WAHITAJI






TTCL jana ilitoa msaada wa vyakula kwa watoto walemavu wa shule ya Msingi Uhuru mchanganyiko pamoja na watoto wasiojiweza wa kituo cha SOS kilichopo kandokando ya barabara ya Sam Nujoma, Mwenge.









Msaada huu wa chakula unalenga kusherehekea sikukuu ya Idd El-Fitr pamoja na watoto hawa ambao kwa namna moja au nyingine ni kundi linalohitaji kusaidiwa na jamii inayolizunguka.







TTCL kama kampuni ya umma na ya kizalendo inajali sana jamii





inayoizunguka pamoja na matatizo yake ndio maanaimeamua kutoa msaada huo wa vyakula kwa makundi haya ya watoto wahitaji ni wazi kuwa ni jukumu letu kama TTCL, kampuni ya kitanzania kusaidia jamii.





Msaada huu kwa vikundi hivi viwili una thamani ya shilingi milio



ni Mbili (2 m/=). Niseme tu kuwa ni utamaduni wetu sisi TTCL kuwa wakarimu si tu kwa kundi hili bali hata kwa makundi mengine yenye mahitaji katika jamii ye



tu ya kitanzania.









Kuthibitisha hilo, Afisa Mtendaji Mkuu





wa TTCL ametoa msaada wa vyakula kwa ajili ya sikukuu ya Idd Elfitr kule Moshi Kilimanjaro kwa vikundi vya wazee, yatima na walemavu wa viungo vya mwili.









Jumla ya vikundi vitatu vitafaidika na msaada wa vyakula wenye thamani ya shilingi milioni moja na laki tano (1.5millioni).









TTCL Inaahidi kuendelea kuhudumia jamii yetu pale kampuni inapofanya vizuri na mapato kuongezeka kwani ndio njia mojawapo ya kurudisha baadhi ya mapato kwa wateja wetu.







Tunashukuru kwa ushirikiano mzuri kati ya TTCL na watanzania Tunaomba tusaidiane kupinga hujuma zozote dhidi ya mtandao na kampuni ya TTCL kwa ujumla.

No comments :

Post a Comment