Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, November 13, 2009

KOMBE LA DUNIA LA TUA KENYA

Raisi Mwai Kibaki na waziri Mkuu Raila Ondiga wakilipokea kombe la Dunia la FIFA (FIFA World Cup Trophy) katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyata JKIA. Mashabikiwa soka hapo kesho watapata nafasi ya kulishuhudia kommbe hilo siku ya Jumamosi katika uwanja wa Nyayo.

Raisi Mwai Kibaki akizungumza katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta amesema ujio wa kombe hilo ni tukio la kihistoria nchini Kenya na nichangamoto kwa taifa hilo katika kuendeleza michezo.Amesema kushinda kombe la Dunia ni ndoto za kila mchezaji na kuwasili nchini Kenya ni nafasi ya pekee ya kuimarisha ndoto na kurekebisha hali ya soka la Kenya amesema Raisi Kibaki.Kibaki, pia amezungumzia nia ya kuunda kamati kufanya kazi ya kuziarika timu zilizofuzu kombe la Dunia kufanya mazoezi nchini Kenya , kabla hazijaenda Afrika ya Kusini.
Amesema kuwa Kenya ina miundo mbinu bora yakuweza kuwasilianan na pande zote za Dunia ni ni masaa machache kwa Ndege kwenda Afrika Kusini.
Raisi Kibaki amesema kufanyika kwa kombe la Dunia kwa mara ya kwanza barani Afrika 2010 kutaifanya Kenya kupata nafasi ya kufaidika kwa Timu nyingi na mashabiki wengi wa Soka watakaopita kwenda Afrika Kusini.
Safari ya kombe la FIFA la Dunia inadhaminiwa na Coca-Cola.
Safari ya Kombe la Dunia ni ya siku 70 katika mataifa 52 ya Africa litaishia Afrika Kusini Desemba 3 huku mataifa 32 yatashirika fainali zijazo za kombe la Dunia.

No comments :

Post a Comment