Klabu ya timu ya Yanga imeitaka mikoa yote ya Tanzania bara kuanza kufanya maandalizi ya uchaguzi wa viongozi katika matawi yake kwa kufuata katiba ya mwaka 2008 ambayo kwa sasa imefanyiwa marekebisho.
Akizungumza na waandishi wa Habari katika Jengo jipya la Timu hiyo yenye maskani yake Jangwani Afisa Habari wa Yanga Luis Sendeu amesema lengo la kufanya hivyo ni kutokana na kuimarisha matawi ambapo kwa kipindi kirefu nafasi nyingi zilikuwa zikikaimiwa.
Sendeu ameongeza kuwa Mchezaji wao Obren Circovic ameondoka jana jioni kuelekea Nchini kwao Serbia kwa ajili ya Kuoa ambapo atakaa kwa wiki mbili.
Lakini pia amesema Mchezaji Nadir Haruob Canavaro ambae amerudi kutoka Cannada baada ya kumaliza mkataba wake wa miezi mitatu kuwa ni mchezaji wao halali mpaka sasa na endapo timu yoyote itamuhitaji basi milango ipo wazi kuzungumza nao kwani bado anamkataba wa miaka miwili.
Akizungumzia kuhusu maendeleo ya timu yake Sendeu amesema Klabu Yanga baada ya kumaliza mchezo wake dhidi ya Tanzania Prison itakuwa mapumzikoni kwa muda wa wiki moja kabla ya kuingia kambini ili kujindaa na Mashindano ya Klabu Bingwa yatakayoaanza Mwezi Januari hapo mwakani.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment