Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, November 3, 2009

YANGA KUANZA MAANDALIZI YA LIGI YA MABINGWA AFRIKA

Klabu ya timu ya Yanga imeitaka mikoa yote ya Tanzania bara kuanza kufanya maandalizi ya uchaguzi wa viongozi katika matawi yake kwa kufuata katiba ya mwaka 2008 ambayo kwa sasa imefanyiwa marekebisho.
Akizungumza na waandishi wa Habari katika Jengo jipya la Timu hiyo yenye maskani yake Jangwani Afisa Habari wa Yanga Luis Sendeu amesema lengo la kufanya hivyo ni kutokana na kuimarisha matawi ambapo kwa kipindi kirefu nafasi nyingi zilikuwa zikikaimiwa.
Sendeu ameongeza kuwa Mchezaji wao Obren Circovic ameondoka jana jioni kuelekea Nchini kwao Serbia kwa ajili ya Kuoa ambapo atakaa kwa wiki mbili.
Lakini pia amesema Mchezaji Nadir Haruob Canavaro ambae amerudi kutoka Cannada baada ya kumaliza mkataba wake wa miezi mitatu kuwa ni mchezaji wao halali mpaka sasa na endapo timu yoyote itamuhitaji basi milango ipo wazi kuzungumza nao kwani bado anamkataba wa miaka miwili.
Akizungumzia kuhusu maendeleo ya timu yake Sendeu amesema Klabu Yanga baada ya kumaliza mchezo wake dhidi ya Tanzania Prison itakuwa mapumzikoni kwa muda wa wiki moja kabla ya kuingia kambini ili kujindaa na Mashindano ya Klabu Bingwa yatakayoaanza Mwezi Januari hapo mwakani.

No comments :

Post a Comment