Mchuano ya Mabara ya Jumuia ya madola iliyopagwa kufanyika Desemba mwaka huu mjini Abuja nchini Nigeria imepigwa kalenda hadi hapo itakapotangazwa tena.
Akiongea na kipindi cha Michezo na Burudani Katibu Mkuu wa chama cha mchezo huo hapa nchini TAHA, Nicolas Mihayo amesema timu ya taifa ya Tanzania imepata nafasi ya kuarikwa katika michuano hiyo pamoja na Cameroon na India.
Amefafanua kuwa kusogezwa mbele michuano kutasaidia kujiandaa vyema katika ushiriki huo kwa kuwa timu ya Tanzania itachaguliwa katika michuano ya Afrika Mashariki na kati yatakayoanza Novemba 14 visiwani Zanzibar.
RAIS DKT. SAMIA SULUHU HASSAN ATOA MKONO WA EID KWA WENYE UHITAJI DODOMA
-
Mkuu Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary S. Senyamule Machi 30,2025 amekabidhi kwa
niaba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Daktari Samia
Suh...
7 hours ago
No comments :
Post a Comment