Waamuzi wanaochezesha Ligi Daraja la kwanza kwa nyakati tofauti wameilalamikia Shirikisho la soka Nchini TFF kwa kushindwa kupatiwa fedha zao kama malipo tangu mwanzo wa Ligi hiyo mpaka sasa.
Mmoja wa Waamuzi hao akizungumza na kipindi cha michezo na burudani wametanabaisha kuwa mara kwa mara wanapuulizia kuhusu posho zao wanaambiwa kuwa wasubiri huku wengine wakiambiwa kuwa tayari wameshalipwa.
Waamuzi hao wamesema wamekuwa wakitupiwa lawama na tuhuma za rushwa katika michezo ya ligi kuu na kupelekea wenzao kufungiwa lakini wamedai TFF inachangia waamuzi hao kupokea rushwa kufuatia kutolipwa posho zao kwa wakati.
Amesema unakuta mwamuzi anatumia fedha zake za mfukoni hadi zinakwisha bila kupatiwa posho ilihali wanasafiri na kulala gesti, na kuhoji vipi wanaweza kujikimu.
Wamesema kuna baadhi ya waamuzi tangu michuano ya ligi daraja la kwanzaimeanza hawajapatiwa fedha zao achilia mbali ambao hawajalipwa malipo ya michezo mitatu, hadi mitano.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment