Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, November 10, 2009

SIMBA, YANGA, AZAM FC NA MTIBWA - TUSKER CUP

Yanga sasa kukutana na Simba kabla ya kuanza duru la pili la ligi kuu Tanzania bara watakapo kutana Desemba katika michuano ya kombe la Tasker Chalenji.
Fredrick Mwakalebela ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la soka Nchini TFF ameyasema hayo wakati akizungumza na Waandishi wa Habari katika ofisi za Shirikisho kuwa vigezo vilivyotumika kuteua vilabu hivyo ni kutokana na msimamo wa Ligi kuu unavyoendelea kwa sasa kwa Timu hizo kushika nafasi za juu.
Klabu zilizochaguliwa kushiriki michuano hiyo ni Simba, Yanga, Azam FC na Mtibwa Suger.
Klabu hizo za Ligi kuu Tanzania Bara zimetakiwa kujiandaa mapema kabla ya kuanza kwa Mashindano ya Tusker Challenge Cup litakapoanza kurindimba hapo Decemba 14 hadi 27 jijini Dar es Salaam mwaka huu.
Wakati huohuo Afisa Masoko wa Tusker ambao ni wadhamini wakuu mashindano hayo Gasto Lyaruu amekabidhi hundi ya kiasi cha shilingi milioni thelathini kwa Shirikisho hilo na kusema wametoa fedha hizo kwaajili ya kuanza kufanya maandalizi mapema ikiwa ni pamoja shughuli za uendeshaji kabla ya Mashindano hayo.

No comments :

Post a Comment