Uongozi wa wekundu wa Msimbazi Simba umeshangazwa na taarifa zilizo enea kuwa klabu hiyo inampango wa kumsajili winga wa Timu ya Yanga Mike Barasa katika dirisha dogo la usajili unaoendelea hivi sasa.
Afisa Habari wa Simba Cliford Mario Dimbo ametanabaisha umma kuwa taarifa hizo si za kweli isipokuwa wanasubiri Kocha Mkuu Patrick Phiri kuwa ni aina gani ya wachezaji atakaowahitaji.
Ndimbo pia amejigamba katika shindano la Tusker Challenge Cup litakaloaanza Decemba kuwa watahakikisha wanalichukua tena kutokana na kikosi chao kusheheni wachezaji wazuri kuliko vilabu vyote vitakavyoshiriki katika michuano hiyo.
Simba kesho inateremka katika dimba la Uhuru kucheza na timu ya Rovu Shooting ikiwa ni mchezo wa kirafiki kocha akiutumia kujaribu wachezaji wake ambao hawakupata nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment