Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Thursday, August 8, 2013

POLISI KUUKABILI UHALIFU KISASA ZAIDI, YAIPA TENDA KAMPUNI YA KIZALENDO YA KOTES (T) LTD KUUNGANISHA VITUO VYAKE VIKUBWA KWENYE MTANDAO WA MAWASILIANO KATIKA MKONGO WA TAIFA




Mkurugenzi wa Kampuni ya kizalendo ya Kotes (T) Ltd, Max Komba (wapili kulia-waliosimama), akikagua uchimbaji mtaro kwa ajili ya kutandika nyanya za mfumo wa mawasiliano kwenye kituo cha Polisi Oysterbay, Dar es Salaam, jana, kuunganisha kwenye mkongo wa mawasiliano wa taifa. Kulia ni Mhandisi wa masuala ya ICT, Makao Makuu ya Polisi,  Mosses Maganza na watatu ni mhandisi wa Kotes (T) Ltd, Mohamed Sibuga.  
HABARI KAMILI
DAR ES SALAAM, Tanzania 
JESHI la Polisi nchini limechukua hatua za kujiimarisha zaidi katika kuukabili uhalifu kisasa zaidi kwa kuamua kuviunganisha vituo vyake vikubwa kwenye mtandao wa mawasiliano katika mkongo wa taifa. 

Kufuatia hatua hiyo, ujenzi wa miundombinu ya mawasiliano hayo ya kuunganishwa kwenye mkongo wa taifa wa mawasiliano, umeshaanza kwenye vituo vikubwa vya polisi katika mikoa ya Mwanza, Arusha, Kilimanjaro, Zanzibar na jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari  jana, Mkurugenzi wa Kampuni ya Kotes (T) Limited iliyopewa na jeshi la polisi kutengeneza miundombinu hiyo, Max Komba, alisema, ujenzi huo ulianza kwenye Kituo cha Polisi Kurasini, Chuo Cha Polisi Chang'ombe na Oysterbay ambako ujenzi wake ulitarajiwa kukamilika jana.

Komba alisema, kampuni yake imepewa kufanya kazi katika mikoa hiyo kwa wiki tatu, tangu ilipoanza Julai 27 mwaka huu kwa mujibu wa mkataba, na ujenzi unatakiwa ume imekamilika ifikapo Agosti 20 mwaka huu.

Likizungumzia mradi huo, Jeshi la Polisi kupitia msemaji wake, lilisema, mradi huo ukikamilika utasaidia jeshi hilo kupunguza gharama na muda mwingi ambao limekuwa likilazimika kutumia katika kufuatilia kumbukumbu katika kuwatambua wahalifu.

Msemaji wa Jeshi hilo, Advera Senso, alisema, kupitia mtandao huo, vituo vilivyounganishwa vinaweza kupata taarifa na kuziona kwa wakati mmoja na kwa haraka zaidi,  jambo ambalo litawezesha kumbaini mhalifu haraka zaidi na kuwa na ushahidi wa kutosha baada ya kumnasa.

"Mradi huu ni miongoni mwa maboresho mengi tunayofanya katika jeshi la polisi ili kwenda na wakati. Hivyo baada ya kukamilisha kwenye vituo vyenye hadhi ya mikoa kipolisi, tunatarajia pia kushuka hadi ngazi za wilaya kulingana na mahitaji", alisema. 

No comments :

Post a Comment