Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Saturday, September 26, 2009

AFRICAN LYON YAFANYA KWELI KAMA LIVERPOOL

HILI NI BENCHI LA UFUNDI LA KLABU YA AFRICAN LYON WA PILI TOKA KULIA NI KOCHA MRENO EDWARD ALMEIDA AKIFUATILIA MCHEZO.
AFRICAN Lyon imezinduka katika mechi ya Ligi Kuu soka Bara baada ya kuilaza Toto African mabao 6-1 kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Huku wakiwa kwenye mvutano na Kocha wao kutoka Ureno, Eduardo Almeida kutoka Ureno kutokana na Lyon kufanya vibaya jana mambo yalibadilika.
Lyon ikiwa na pointi moja baada ya mechi nne jana ilicharuka na huku ikiongozwa na Mremo huyo ambaye baadhi ya vyombo vya habari viliripoti amefukuzwa iliibuka na ushindi mkubwa tangu ligi hiyo ianze msimu huu.
Timu hiyo yenye makazi yake Mbagala iliwanyanyasa watoto wa Yanga, Toto kama ilivyofanya Liverpool kwa Hull City katika Ligi Kuu ya England jana kwa kushinda 6-1.
Bao la African Lyon lilipatikana dakika ya kwanza kwa shuti la mpira wa adhabu uliopigwa na Rashid Gumbo na kumshinda kipa Hussein Katandula.
Dakika ya 29, Robert Sentongo aliifungia Lyon bao la pili baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Idrisa Abdallah.
Toto ilipata bao la kwanza dakika ya 61, lililofungwa na Maulid Hanim baada ya kuwalamba chenga mabeki wa Lyon na kuusukumia mpira wavuni.
Hata hivyo, furaha yao ilizimwa dakika moja baadaye kufuatia bao lililofungwa na Yusuph Soka baada ya kuwatoka mabeki wa Toto na bao la nne lilifungwa pia na Soka.
Mbwana Samatta aliipatia Lyon bao la tano na dakika ya 74 na dakika ya 83, Samata alifunga bao la sita.
Mara baada ya mechi hiyo kumalizika, Kocha Mkuu wa Toto African, Mbwana Makatta, alisema tangu aanze kuifundisha timu hiyo, hajawahi kupata kipigo kama hicho.
Makatta alikiri kuzidiwa na African Lyon na kwamba yote hayo yamesababishwa na baadhi ya wachezaji kuwa na matatizo na uongozi na wengine walipata kadi nyekundu.

No comments :

Post a Comment