Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Friday, September 11, 2009

SEMENYA ANA JINSIA MBILI ???

Vipimo kwa bingwa wa Dunia katika mbio za mita 800 raia wa Afrika Kusini Caster Semenya hadi sasa bado vinautata lakini baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiandika kuwa anajinsia mbili ya uke na ume.
Semenya, mwenye umri wa miaka 18, ambaye aliombwa kufanyiwa vipimo ili kubaini jinsia yake kufuatia kuwashangaza watu katika michuano ya Dunia ya riadha mwaka huu na masaa machache kabla ya kushinda huko Berlin.
Magazeti ya Australia yamedai kwamba Semenya ni mtu mwenye jinsia moja lakini anahisia za jinsia nyingine ama ana jinsia zote mbili kitaalamu wanaita hermaphrodite.
Waziri wa Michezo Makhenkesi Stofile amesisitiza mapema leo kwamba "Caster is a woman, she remains our heroine. We must protect her."
Naye Raisi wa Riadha wa Afrika Kusini Leonard Chuene ameliambia gazeti la Star: kwamba IAAF wamewaambia matokeo ya vipimo yanatatanisha hivyo hawawezi kuwapataia.
Mwenyekiti wa Baraza la taifa la michezo, Butana Komphela ameongeza kuwa "Someone is guilty of leaking her confidential medical information to Australian newspapers."
IAAF imethibitisha kuwa kwa sasa haitatoa kauli yeyote kuhusu Semenya hadi wakati mkutano wa kamati ya utendaji ya IAAF itakapokutana Monaco Novemba 20-21.
Semenya alitwaa uchampion wa Dunia wa mita 800 mjini Berlin mwezi August kwa kuweka rekodi ya kukimbia dakika 55.45, akiwa mbele kwa dakika 2.5 dhidi ya bingwa wa mwaka 2007 Mkenya Janeth Jepkosgei.

No comments :

Post a Comment