Shirikisho la kandanda hapa nchini TFF, limeandaa semina ya siku 2 kwa Makatibu wakuu 12 wa vilabu vinavyoshiriki Ligi kuu Tanzania Bara ya Vodacom itakayofanyika katika ofisi za Shirikisho hilo kuanzia Septemba 24 hadi 25 mwaka huu.
Akizungumza na kipindi hiki Afisa Habari wa TFF Frolian Loimamu Kaijage amesema lengo la kufanya hivyo ni kuwapiga msasa kuhusiana na masuala mbalimbali ikiwa sambamba na kufahamu majukumu yao ya kazi.
Kaijage ameongeza kuwa semina hiyo itaongozwa na Mkufunzi ambae pia ni Mjumbe wa Fifa Henry Tandau.
Wakati huo huo, Kaijage amewataka wadau na wapenzi wa mpira wa miguu wawe na subira kuhusiana na lawama wanazopelekewa Waamuzi kutokana na uchezeshaji mbovu unaotokea katika mzunguko mzima wa ligi kuu.
BONDIA RAMADHANI MIGWENE AMUWEKEA MIKWALA ALBANO CLEMENT BAADA YA KUKIMBIWA
NA HABIBU PENGO
-
BONDIA RAMADHANI MIGWEDE baada ya kukimbiwa na mpinzani wake Habibu Pengo
aliesaini nae kuzipiga mara ya kwanza sasa amebadilishiwa mpinzani na
atacheza na...
2 years ago
No comments :
Post a Comment