Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Monday, May 16, 2011

BINGWA WA OLIMPIKI SAMUEL WANJIRU AFARIKI

Samuel Wanjiru

Samuel Wanjiru mshindi wa marathon Olimpiki 2008

Bingwa wa Olimpiki katika mbio za masafa marefu za Marathon Mkenya Samuel Wanjiru ameaga dunia.

Duru za polisi zinasema, Wanjiru alikumbana na mauti baada ya kuruka kutoka kwenye chumba chake cha ghorofa moja eneo la Nyahururu, mkoa wa Kati wa Kenya.

Idara ya polisi imethibitisha kifo hicho na kusema uchunguzi umeanzishwa ili kubainisha sababu za kifo hicho.

Mwanariadha huyo alishinda medali ya dhahabu katika mbio za Olimpiki mwaka 2008 mjini Beijing, kwa kuweka muda wa 2:06:32. na kuandikisha rekodi ya kuwa Mkenya wa kwanza kushinda mbio za marathon kwa upande wa wanaume .

Wanjiru pia alikuwa bingwa wa ulimwengu katika misururu ya mbio za marathon maarufu kama world marathon ,ajors kuanzia mwaka 2008 hadi mwaka 2010.

Wanjiru pia aliweka rekodi ya mbio za kilomita 21 kwa kuandikisha muda wa dakika 58:33.

Mwezi DeSemba mwaka uliopita Wanjiru alifikishwa mahakamaNI, kwa mashtaka ya kutishia kumwuua mkewe, kumjeruhi mlinzi wake wa nyumbani na pia kumiliki bunduki aina ya AK-47 bila idhini ya serikali.

Mapema mwaka huu Wanjiru alipata ajali mbaya katika barabara inayotoka Nairobi kuelekea Nyahururu, hatua iliyomfanya kujiondoa kutoka kwenye mbio za London Marathon.

No comments :

Post a Comment