Tangazo

Sikiliza kipindi cha michezo kutoka CAPITAL RADIO kilasiku 21:00


Viwanjani%20%28Maximo%29
Quantcast

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI

TANGAZO LA UPATIKANAJI WA VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI
VIFAA VYA MCHEZO WA NGUMI PAMOJA NA DVD ZA MAFUNZO SASA ZINAPATIKANA MAKUTANO YA BARABARA YA UHURU NA MSIMBAZI DAR ES SALAAM KARIAKOO ZAIDI WASILIANA NA SUPER D SUPER COACH KWA NAMBA YA SIMU 0713406938 Rajabu Mhamila 'Super D' Photojournalist at Majira, Business Times Email.superdboxingcoach@gmail.com mhamila1@gmail.com www.superdboxingcoach.blogspot.com Mob;+255787 406938 +255774406938, +255713406938 Po.Box. 15493 Dar es Salaam Tanzania

Tuesday, May 17, 2011

TAARIFA TOKA SHIRIKISHO LA KANDANDA TANZANIA TFF

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mei 17, 2011

KITUO CHA KUKUZA VIPAJI CHA TSA
Kituo cha kukuza vipaji cha Tanzania Soccer Academy (TSA) kinachoendeshwa kwa
ubia kati ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na kampuni ya Kiliwood
kimesimamisha shughuli zake tangu mwaka jana.

Kamati ya Utendaji katika kikao chake cha kwanza mwaka huu ilishafanya uamuzi
juu ya uendeshaji wa kituo hicho na kutoa maelekezo kwa Sekretarieti ya TFF. Kwa
vile kituo hicho kilichokuwa kinachukua vijana wenye umri kuanzia miaka 17 hadi
20 ni cha ubia kati ya TFF na Kiliwood uamuzi wowote juu ya mustakabali wake ni
lazima uhusishe pande hizo mbili.

Kwa mantiki hiyo Sekretarieti kwa sasa inafanya mawasiliano na kampuni ya
Kiliwood ili pande hizo mbili zikutane na kuelezana juu ya uamuzi wa Kamati ya
Utendaji ya TFF juu ya mustakabali wa kituo hicho.


Wajibu wa TFF katika mkataba kati yake na Kiliwood juu ya uendeshaji wa kituo
hicho ni vitendea kazi (facilities) ambavyo ni hosteli na uwanja wa mazoezi.


KOZI YA WAKUFUNZI WA MAREFA
TFF kupitia Kurugenzi ya Ufundi imeandaa kozi ya wakufunzi wa marefa wa mikoa
itakayofanyika Dar es Salaam kuanzia Juni 1 hadi 4 mwaka huu.

Kozi hiyo inatarajia kushirikisha wakufunzi wa marefa zaidi ya 20 kutoka mikoa
yote ya Tanzania Bara. Mara ya mwisho kozi hiyo ilifanyika nchini mwaka 2008.


Wawezeshaji katika kozi hiyo ni Stanley Lugenge ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati
ya Waamuzi ya TFF, Leslie Liunda, Joseph Mapunda, Hafidh Ally na Juma Hamisi.

Boniface Wambura
Ofisa Habari TFF

No comments :

Post a Comment